Monday, January 31, 2022

MITIHANI YA SHULE ZA MSINGI

 

MTIHANI WA DARASA LA II

SOMO: KUHESABU

 


Andika namba hizi kwa Tarakimu

1. Mia tano………………………

2. Mia nne tisini……………………

3. Mia tatu………………………….

4. Mia mbili na ishirini………………

5. Elfu moja……………………………..

6.    3  2  5
+ 1  4  3
  _____
       

7.    7  1  6
+ 2   3  1
______

8.   5  6 1
+ 4 2 3
_____

9.    1 2 8
+ 2 8 3
______

10.    3 3 6
+  4 8 6
_____

11.     635  - 213 =

12.    287  + 113 =

13.    6  2 4
_   3  2  1
______

14.    9 7 5
_   2  3 0
______

15.    5 7 6
-   2 6 8
______

Andika sehemu iliyotiwa kivuli

16.   
                                                                             
                                        

17.                                                                  
                                                    
                                            

18.                                               
                 

19.                                 

20.         Namba   mamia   makumi    mamoja
      263      …………       ………..          …………


SHULE YA AWALI NA MASOMO YA ZIADA

 

SHULE YA AWALI NA MASOMO YA ZIADA YA BRIGHT

MTIHANI  WA HISABATI WA MAJARIBIO

IJUMAA 12/11/2021

MUDA: SAA 1

 

JIBU MASWALI YOTE.

 

ANDIKA NAMBA ZIFUATAZO KWA TARAKIMU

1. Themanini na nne…………………………

2. Tisini na tisa……………………………….

3. Thelathini na tano………………………..

ANDIKA NAMBA ZIFUATAZO KWA MANENO

4. 27=…………………………………………………….

5. 3/4 =…………………………………………………..

6. 33=…………………………………………………..

ANDIKA NAMBA ZINAZOKOSEKANA

7. 3,  4,  5,      ,    7,            ,    9 
 

8. 12,   14,  16,          20,      , 24,       , 30     

9.   31  +  4 =   

10.   48  -  18=

11.   87  - 49 =

12.    7 9
+
1 2
   ___

13.    6 8
- 
2 9
   ___

14.   6 4
+1 6
____

15.   9 8
- 1 9 
____ 

16.   342   +  436  =

17.    3 5 6
+ 2 7 5
_____ 

18.   247  -  123 =

19.  7 2 8
-4 0 9
____ 

20. 2  X   8=

21. 3   X   4 =

Umbo hili linaitwaje?             

Sunday, January 30, 2022

SOLUTION TO RESOLVE GREAT DEPRESSION IN COLONOES

 1.Introduction of labour instate 

2.Land conservation programmed 

3.Emphasis peasant economy 

4.Imrove of infrastructure 

5.Launching progressive farmers 

6.To ontroduce focal point approach peasant we're given assistance by the colonial 




EFFECT OF GREAT DEPRESSION IN AFRICA

 1.Drastically fall of price of cash crops 

2.Reduction in provi 

7.Increase of low wages to workers 

8.Intensive nature of seggregation and exploitationsion of social services 

3.Massive unemployment 

4.Higher level of emphasis of cash crops 

5.Intensively land annotation and propertie

CAUSES OF GREAT DEPRESSION

 1.Protection 

2.The impacts of Russia revolution 

3.Post war economic recoveries in Europe 

4.Over production 

5.Collapse of New York stock exchange 

6.Nature of the economy with business cycle 

7.Bank failures 

8.Uneven distribution of income

EFFECTS OF FIRST WORLD WAR ON AFRICA

 1.Spread and occurrence of diseases 

2.Intensifications of exploitation to the African 

3.Hunger and starvation 

4.The rise of great depression 

5.Emergence of league of nation 

6.Decline of agricultural production 

7.Poor social services for Africa 

8.Death of African soldiers

CAUSES OF FIRST WORLD WAR

1. Development of capitalism to highest stage.2.Militarism in Europe.3.Formation of antegonestic alliance in Europe.4.Economic competition among imperialist power.5.Assassination in Sarajevo Archiduke

CRISES IN THE CAPITALIST SYSTEM

 THE RISE OF FIRST WORLD WAR 1914-1918.The first world war was an imperialist war which had it's roots in European imperialist activities in Europe,Asia and Africa.The war broke out due to an agonistic classes two imperialist camp as control power-.Germy,Italy,Austral-Hungary and Turkey and allied power- Britain,France,Russia, and USA.The first world war broke out from 1914-1918 accelerate d with the association of Archduke Ferdinand and his wife by when they visit Ed Bosnia the capital of Sarajevo

Saturday, January 29, 2022

MAOMBI YA KUJIKOMBOA

 MAOMBI ya KUJIKOMBOA                              Kila mshale was mauti,magonja nauteketeza 

Kwa jina la Yesu.kila ukuta was laana juu yangu nauangusha Kwa jina la Yes.kila roho ya mauti na magonjwa pigwa Kwa jina la Yes.kila shimo la mauti na magonjwa teketea Kwa jina la Yes.kila mateso maishani mwangu toweka ka jina la Yes.kila nguvu ya kifo pigwa Kwa damu ya Yesu.nakataa Kila ugonjwa na shida kwenye maisha yangu Kwa jina la Yes.nafsi yangu pokea uponyaji Kwa damu ya Yes.kila mbegu ya mauti toweka Kwa jina la Yesu.kila wakala was mauti pigwa Kwa jina la Yes.kila funza was mauti na magonjwa nakuchoma Moto Kwa jina la Yesu

Kila matatizo kwenye maisha yangu toweka Kwa jina la Yesu


Friday, January 28, 2022

KUEPUKA UZINZI, NA UASHERATI NDANI YA WOKOVU.

  

KUEPUKA UZINZI, NA UASHERATI NDANI YA WOKOVU.

 

Uzinzi: Ni kitendo cha mume au mke kutoka nje ya ndoa yake na kuwa na mahusianoya kimapenzi na mwanamke au mwanaume mwingine (kufanya tendo la ndoa nje ya ndoa) Mungu anatukataza kwamba tusizini .

“Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine naam yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye na mwanamke hakika watanawa”. Walawi 20:10

 

Usilale na mke wa mwenzio ukajitia unajisi naye.Walawi 18 :20

 

Uasherati: Ni kitendo cha watu wasio olewa au kuoa ambaye atafanya mapenzi kabla ya ndoa. Mungu anakataza sana.

“mtu yeyote wa kwenu asimkaribie mwenziwe alie wa jamaa yake wa karibu ili kumfunua utupu mimi ndimi BWANA”. Walawi  18:6  

 

Kwa hiyo utaona ukisoma kitabu cha mambo ya walawi sura ya 18:1-23na 20:1-21 Mungu anavyokemea uzinzi na uasherati kwa nguvu zote, kwa kufafanua kwa uwazi. Ndani ya kanisa na nje ya kanisa tunatakiwa kuikimbia zinaa kwa nguvu zetu zote, maana sisi ni hekalu laMungu lazima mipaka (kujiwekea mipaka) kwa jinsia tofauti ili kuepuka uzinzi na uasherati kwetu. Kweli tumeokoka na tutaenda mbinguni.

Lakini kama hatutaitiisha miili yetu kwa uzinzi na uasherati hatutaenda mbinguni. Kijana wa kiume na wakike mnatakiwa kujilinda na kujichunga )sio vijana tu na watu wote) maana uzinzi na uasherati hauchagui umri  usiseme mimi ni mwombaji sana na ninaupako sana lakini bila kuwa makini unaweza kuangukia huko.

 

MAMBO YA KUFANYA KUEPUKA UZINZI NA UASHERATI

1.     Kuwa muombaji:

Unapokuwa muombaji mbele za Mungu inasaidia kuepuka usiingie kwenye majaribu au jaribu la uzinzi.

“Kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni roho i radhi lakini mwili ni dhaifu” Mathayo.

2.     Kuepuka mazingira hatarishi.

Ukishaona mazingira uliopo ni ya hatarishi yananukia uzinzi au uasherati kimbia, Mfano:ukishaona mtu anakuonyesha dalili hizo usiseme mtaomba cha kufanya kimbia.

“Ikimbieni zinaa kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake ili yeye afanyae zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe”. 1 Wakoritho 6:18

3.     Jiepushe na mavazi ya kikahaba:

Kimsingi shetani yupo na anatenda kazi wewe mwanamke na mwanaume jiepusheni kuvaa mavazi yasio mpendeza Mungu(yasiyo na utukufu wa Mungu). Mavazi hayo yanachochea uzinzi na uasherati kwa watu.

“Je humjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha” 1Wakoritho 6:15

 

 

4.     Kuwa na hofu ya Mungu:

Unapo kuwa na hofu ya Mungu, itakusaidia sana utajua kama utatenda uzinzi au uasherati  utakuwa unamkosea Mungu aliekuokoa, maana sisi ni hekalu la Mungu(Roho Mtakatifu)

“ Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi mtukuzeni Mungu katika miili yenu” 1Wakoritho 6:19-20

 

 

5.     Kujiepusha na vitendo vya ushawishi: kikawaida kuna vitendo ambavyo vinaweza kuwapelekea au vikachochea uzinzi au uasherati. Mfano: kuchati muda mwingi na jinsia tofauti kwa kuitana majina ambayo hukutakiwa kuyasema au kuwa na muda mwingi na jinsia tofauti kutembeleana nyumbani peke yako ni hatari sana shetani anaweza akawaingia mkafanya uovu. Ni vyema mkawa zaidi ya mmoja.

“Basi palitokea mashindano baina yao hata wakatengana, Barnaba akamchukua Marko akatweka kwenda kipro, lakini Paulo akamchukua sila, akaondoka akiombewa na wale ndugu apewe neema ya Bwana” Matendo 15:39-40

 

6.     Kufanya mazoezi ya mwili:

Mazoezi ni muhimu sana kwa ajili ya afya yako. Ni vema ukafanya mazoezi ili kuepuka zinaa.

“Je hamjui yakuwa wale washindanao kwa kupiga mbio wote, lakini apokeae tuzo pigeni mbio  namna hiyoili mpate”1wakoritho 9:24

 

 

7.     Kujiweka bize

Unapokuwa bise katika kumtafakari Mungu na neno lake au ukuu wake itakusaidia sana. Mfano:Kama wewe ni mwanafunzi jiweke bize katika kujisomea masomo yako.

“nimevipiga vitu vilivyo vizuri mwendo nimeumaliza imani nimeilinda”.2timotheo 4:7

 

8.     Jitambue wewe ni kielelezo kwa Mungu:

Unapo okoka unatakiwa uwe ni kielelezo mbele za Mungu na mwanadamu. Kama utasema umeokoka na ujihusisha na maovu hapo unakuwa unamtukanisha Mungu.

“Katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema na katika mafundisho yako ukionyesha usahili na usahivu”. Tito 2:7

 

MADHARA YA ZIINAA( Uzinzi na uasherati)

Usisahau dhambi ni kazi na ni lazima ulipwe (mshahara lazima ulipwe)

“kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti bali karama ya Mungu nai uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu” Warumi 6:23

                                             i.            Zinaa inaua utu wa ndani.

“Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili” Mithali 18:14

Zinaa inajeruhi na kuumiza mtu wa ndani na kumuangamiza nafsi yake.

 

“Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa, afanya jambo litakalo mwangamiza nafsi yake” Mithali 6:32

                                           ii.            Humvunjia mtu heshima na kupata fedheha.

“Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima wala fedheha yake haitafutika”Mithali 6:33

              iii.            Inafuta maono na ndoto zako(utamkosa Mungu ) Yusufu alijua kwamba amebeba maono ya Mungu na ndiyo maana mke wa bosi wake alipotaka kufanya naye mapenzi alikimbia.

“Ikiwa baada ya mambo hayo mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia lala nami. lakini akakataa------------- Mwanzo 39:6-12

“Nifanyeje ubaya huu mkubwa nimkosee Mungu?Mwanzo 6:9

              iv.            Humwaondolea mtu ujasiri wakukemea dhambi.

Mtu anakosa ujasiri mbele ya Mungu na wanadamu kwa sababu moyo wako unakuhukumu.

“Wapenzi mioyo yetu isipotuhumu tunaujasiri kwa Mungu” 1Yohana 3:21

                 v.            Huleta muunganiko wa mwili.

“Au haujui yakuwa yeye aliyeungana na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema wale wawili watakuwa mwili mmoja” 1wakoritho6:16

Kumbuka hili ni agano(zinaa ni agano) au unaweza kusema ni kifungo unaunganisha,mwili, nafsi na moyo (roho yako) ndiyo maana utakuta mtu kabla ya kuokoka alikuwa na mtu wake (mpenzi)unakuta wameokoka wanaendelea na zinaa kama mwanzo.


              vi.            Hukiingiza kizazi chako kwenye vifungo

“Baba zetu walitenda dhambi hata hawako na sisi tumeyachukua maovu yao” Maombolezo 5:7

 

            vii.            Huambukiza magonjwa.

Zinaa inaweza kukuambukiza magonjwa ya namna mbalimbali.

 

         viii.            Ni mlango wa mapepo kwa wanadamu.

 

              ix.             Inaua kiroho na kimwili

“Ndipo Bwana akanyosha juu ya sodoma na juu ya gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa Bwana” Mwanzo 19:24.

 

     x.            Inaweza kukufanya usiurithi ufalme wa Mungu (ukafutwa kwenye kitabu cha uzima)

“Bali waoga na wasio amini na wachukizao na wauaji na wazinzi na wachawi na hao waabuduo sanamu na waongo wote sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberit. Hii ndiyo mauti ya pili”

“Na iwapo mtu yeyote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima alitupwa katika hilo ziwa la moto”Ufunuo 20:15

 


KAMA HUJAOKOKA SEMA MANENO HAYA KWA KUYAKIRI NA KUYAAMINI MOYONI MWAKO.

 

Baba Mungu katika jina la Yesu Kristo nakuja mbele zako, mimi ni mwenye dhambi ninaomba unisamehe dhambi zangu zote nilizozitenda kwa kujua au kwakuto kujua na ninazo zikumbuka na nisizo zikumbuka. Ninaomba unirehemu, ninaomba unihurumie mimi mwenye dhambi, ninakuomba futa jina langu kwenye kitabu cha hukumu na uandike jina langu kwenye kitabu cha uzima. Ninaomba uwe Bwana na mwokozi wa maisha yangu, naomba unipe neema niwe mwaminifu mbele zako na hata milele. Asante Yesu Kristo kwa kunisamehe dhambi zangu. Nimekuwa kiumbe kipya mbele zako, katika jina la Yesu kristo. Ameni

 

Niseme kwamba Mungu amekusamehe dhambi zako wala azikumbuki tena endelea kujifunza neno la Mungu ili neema uliyoipata isipotee. Sasa wewe ni kiumbe kipya ndani ya Kristo Yesu yakale yamekwisha tazama ni mapya ni katika jina la Yesu. Wokovu ulioupate ni wa thamani sana na hiyo ndiyo tiketi ya kwenda mbinguni.

 


 

MUNGU AKUBARIKI.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

AHADI ZA MUNGU KWETU.

 

 

AHADI ZA MUNGU KWETU.

Ahadi. Ninamna Fulani ya kusubilia au kutarajia kile unachokihitaji , mfano, ninakuahidi ile fedha nitakupa wiki ijayo. Kwa hiyo ahadi kwa namna nyingine ni kama kiapo, Hivyo tunafahamu Neno la Mungu limehakikishwa na Mungu mwenyewe ni hai tena linanguvu, kuna umuhimu wa kulitumia Neno la Mungu na ahadi zake wakati wa maombi Na Mungu huwa analiangalia Neno lake ili alitimize.

Na wewe kama mwombaji unatakiwa kuzijua na kuzitumia ahadi kwa kumkumbusha Mungu anachosema katika Neno lake ili kusababisha mabadiliko mazuri yatokee katika ulimwengu wa mwili kama tunavyoomba,

 

‘Unikumbushe na tuhojiane eleza mambo yako, upate kupewa haki yako ‘Isaya 43;26.

 

AHADI ZA MUNGU JUU YETU.

Kuna ahadi za Mungu juu yetu zaidi ya elfu thelasini na sita (36,000) Lakini zifuatazo hizi ni baadhi tu.

 

i)Ahadi za Mungu kuhusu mamlaka aliyotupa sisi.

“Tazama nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge na nguvu zote za Yule adui” Luka 10;19

 

ii) Ahadi za Mungu za kumshinda shetani na nguvu za giza

“Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana- simba na joka utawaseta kwa miguu “Zaburi 91;13

 

 

iii)Ahadi za Mungu kuhusu uponyaji wa magonjwa.

Ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya akisema, mwenyewe alimtwaa udhaifu wetu, na kuyachukua magonjwa yetu. ‘Mathayo 8;17.

i)                   Ahadi za Mungu kuhusu ulinzi na usalama

‘Bwana  ndiye mlinzi wako ,Bwana ni uvuli ,mkono wako wa kuume, Zaburi 91;5.

 

ii)                Ahadi za Mungu kuhusu akili njema,

maarifa  ‘Yafahamu sana hayo nisemayo kwa maana Bwana atakupa akili katika mambo yote. 2timotheo 2;7.

 

iii)              Ahadi za  Mungu kuhusu utajiri na mafanikio

Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako kama vile Roho yako ifanikiwavyo 3Yohana 1;2

 

Kwa maana hakuna tofauti ya myahudi, maana yeye Yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao,warumi 10;12.

iv)              Ahadi za Mungu kuhusu watoto na familia,

‘Na watoto wako wote watafundishwa na Bwana na amani ya watoto itakuwa nyingi, Isaya 54;13.

 

MAMLAKA YA KUTAWALA, KUTIISHA NA KUMILIKI.

Mamlaka ; Ni nguvu aliyonayo mtu kutokana na (kuhusiana) na jambo Fulani.

‘Mungu akasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu,kwa  sura yetu wakatawale samaki wa bahari na ndege wa angani na wanyama na nchi yote pia na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanake aliwaumba. Mungu akawabarikia, Mungu akawambia zaeni mkaongezeke, mkazazike, mkaijaze nchi na kuitiisha, mkatawale samaki wa baharini na ndege wa angani na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi. Mwanzo 1;26-28.

 

*Akawabariki.

Hapa Mungu aliachilia nguvu ndani yao na juu yao ya kuzipata hizo Baraka,

*Zaeni mkaongezeke,

Maana yake ndani ya mtu Mungu ameweka mbegu za Baraka na za uzao.

 

Lengo la Mungu kumuumba mtu ili aweze kutawala, kumiliki na kutiisha vyote ambavyo ni dhana ya ufalme.

 

Msiogope enyi kundi dogo kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme”,Luka 12;32

 

Nami nawawekea ninyi ufalme kama vile Baba yangu alivyoniwekea mimi, Luka 22;29.


 

Mfalme anawatawala kwa kutumia neno / amri

‘Kwa kuwa neno la mfalme lina nguvu naye ni nani awezaye kumwambia huyo, wafanya nini? Mhubiri 8;4.

 

‘Na mbarikiwe ninyi na Bwana aliyezifanya mbingu na nchi, Zaburi 115;15-16

Na mfumo ambao Mungu ameuweka wa mtu kumiliki juu ya nchi ni kwa njia ya ufalme na ukuhani.

Ukuhani; Unafanya kazi ya utakaso na toba ili kuweza kuunganisha mbingu na nchi.

 

Na kutufanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu naye ni Baba yake, utukufu na ukuu una yeye hata milele na milele.Amina. Ufunuo 1;6.

Kila mahali zitakapokanyaga nyayo zangu nimemiliki sasa mbona shida, taabu, matatizo, mikosi,n.k, suala hapa unakanyagaje?Lazima ukanyage kikuhani na mkanyago wa kifalme kwa kusema neno la Mungu juu ya mahali hapo ulipo (Ardhi)

 

Katika siku zile mimi Daniel nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamiliDaniel 10;2.

Fahamu ardhi ya eneo linapomilikiwa na adui kunakuwa na kukatika kwa mawasiliano kati ya mbingu na ardhi. Baraka za Mungu zinakuwa ngumu sana kukifikia kwasababu ya mkuu wa anga (pepo) atakuwa anazuia kila jema kutoka mbinguni.

Kwahiyo wewe lazima ujitambue kwamba wewe upo ndani ya ufalme wa Mungu. Na unapozungumzia ufalme lazima mfalme awepo.

Ufalme. Ni mfumo wa utawala (ni serikali)

Mfalme. Ni mtawala aliyepata nguvu za utawala kwa njia ya urithi au uwezo Fulani.


Na alipoulizwa na mafarisayo Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza, wala hawakusema tazama upo huku au kule kwa maana,tazama ufalme wa Mungu umo ndani yenu Luka 17;20-21

 

Yesu akajibu  ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangenipigania nisije nikatiwa mikononi mwa wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa, Basi pilato akamwambia, wewe u  mfalme basi? Yesu akajibu wewe wasema kuwa mimi ni mfalme ,mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya na kwa ajili ya haya mimi nakuja ulimwenguni ili nishuhudie kweli. kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu, Yohana 18;36-37.

 

Unapouzungumzia ufalme unazungumzia,

*mamlaka

*uwezo

*kumiliki

*kutiisha

*utawala

 


 

MUUNGANIKO WA MTU NA MBINGUNI.

Baada ya kuokoka,  kutubu dhambi zako. Sasa Mungu amekuunganisha kwenye ufalme wake na una haki zote za msingi kuzungumza na Mungu au kumdai, ahadi zake kwako.

 

Muunganiko, Ni uhusiano uliopo kati ya mmoja na mwingine au ni muunganiko wa mtu na kitu au vitu.

 

Mbinguni, Ni makao makuu ya Mungu na malaika zake watakatifu, maana yake hapa tunazungumzia

a)Mungu Baba.

b)Mungu Mwana.

c)Mungu Roho Mtakatifu

d)Malaika wake (malaika wa Mungu).

 

“Baada ya hayo naliona na tazama mlango ukafunguka mbinguni na sauti ile ya kwanza ukafunguka kama sauti ya baragumu ikinena nami ikisema panda  hata huku nami nitakuonyesha mambo magumu ambayo huyana budi kuwako baada ya hayo. Na mara nalikuwa  katika Roho na tazama kiti cha enzi kimewekwa mbinguni na mmoja ameketi juu ya jiwe la yaspi na akiki na upande wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi ukionekana mithili ya  Zumaridi. Ufunuo 4;1-11.

Ukiendelea kusoma mpaka mstari wa kumi na moja uatona kuna wazee ishirini na wanne, kiti cha enzi, taa saba za moto. (Roho saba za Mungu)

 

1.     Kiti cha enzi; Hiki ni kiti cha Mungu Baba aliyeziumba mbingu na nchi.

2.     Wazee ishirini na nne,  Hawa ni  viongozi wa kiroho kanisani.


3.     Taa saba za moto (Roho saba za Mungu)

*Roho ya ushauri

*Uweza

*Kumcha Bwana

*Maarifa

*Hekima

*Ufahamu

*Kuonya

 

            4. Wenye uhai wanne

     a). Mfano wa simba; maana yake ni roho ya         mapambano 

b)Mfano wa ndama; maana yake ni roho ya utayari kwenye kazi ya Mungu

c)mfano wa mwanadamu; maana yake  ni roho ya upole na huruma.

d) Mfano wa tai arukae; maana yake ni macho ya kinabii (kuona mbali) (prophetic eyes)

5. Maneno (sauti)

*mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu Bwana Mungu mwenyezi.

*Umestahili wewe bwana wetu na Mungu wetu.

*Kuupokea utukukufu na heshima na uweza.

*Wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote,

*Kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako navyo vikaumbwa.

6. Matendo waliyokuwa wanayafanya.

*Wanatoa utukufu na heshima na shukrani

*Walikuwa wakipiga magoti.

*Wakimsujudia yeye aliye hai.

 

Kwa hiyo tunakuwa tumeunganishwa au tunamuunganiko na mbinguni.

 

“Hata petro alipopata fahamu akasema, sasa nimejua ya kini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la wayahudi. Matendo 12;11.

 Vilevile sisi tuliookoka na kumtumainia Mungu tunapaswa kuelewa ziara za malaika kwamba wanapanda na kushuka wakati gani.

 

Akaota ndoto na tazama ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni na kushika juu yake, Mwanzo 28;12.

 Tunaona Yakobo alikuwa amelala usingizi akaota ndoto hiyo na hapo jua lilikuwa limezama (sura ya 28;11). Hivyo basi kumbe tunapoomba usiku ndiyo ratiba za malaika wanakuwa wanapanda na kushuka, kwa ajili ya kuchukua maombi yetu na kuyapeleka mbinguni kwa Baba, (sio kwamba mchana hawapo , wapo pia.)

Sisi ni watoto wa Yesu Kristo na tunahitaji nguvu za Yesu zijizihirishe kwetu kwa kumshinda shetani na malaika zake tunapaswa kuomba usiku wa manane. Kanisa letu la Tanzania Power of Jesus Christ, tunatakiwa tuwe na nguvu za Rohoni. Kwasababu mchana tunashughuli nyingi ni vema tukautumia muda huo wa usiku kuanzia saa 6 na saa 11 alfajiri hapo utazipata nguvu za Yesu Kristo, Halelluya!!.

 

 

BARAKA ZA TOKA ULIMWENGU WA ROHO.

Baraka; Ni mafanikio ya mtu aliyonayo kiroho au kimwili. Lakini kwenye ulimwengu wa roho wa Mungu Baba, Baraka zipo nyingi sana ila tunashindwa kuzitoa huko na kuja kwetu kwenye ulimwengu wa mwili, kwahiyo Baraka zozote iwe ni fedha, huduma, mashamba, magari, nyumba, chakula,  kazi, ndoa, biashara, elimu, watoto n.k zote hizo zipo kwenye ulimwengu wa roho.

 

“Atukuzwe Mungu Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo aliyetubariki kwa Baraka zote za rohoni katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo. Waefeso 1;3.

 

Mfano;  Unataka kupata Picha au sauti (taarifa ya habari) lazima uwe na vitu vifuatavyo.

 

a)    Tv (runinga)

Maana yake hapa, unatakiwa uwe na Yesu ndani ya moyo wako (umeokoka)

 

b)    King’amuzi.

Hapa hitaji lako ni nini kwa Mungu Baba unalolihitaji, je  ni fedha, kazi, ndoa n.k.

 

c)     Umeme

Hapa unatakiwa kuwa na nguvu za Roho Mtakatifu.

 

d)    Muunganiko (connection)

Hapa unahitajika kuwa na Neno la Mungu ndani yako.


e)     Sigino (signal)

Hapa unatakuwa upate sehemu sahihi ya kumuabudu Mungu Baba ili baraka zako uzione na kuzipata.

f)      Remote.

Hapa ni Yule anayekuongoza (baba yako wa kiroho) anatakiwa kuwa na nguvu za kiroho ili atakapokubariki baraka ikufuate na sio kukutamkia laana.

Mungu yeye siku zote anatenda mambo ya ajabu mno kuliko yote,

*Tuyaombayo

*Tuyawazayo

*kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu (yako).

“Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo kwa kadri ya nguvu itengayo kazi ndani yetu .Waefeso 3;20.

 

BIBLIA INAFUNDISHA.

1.     Ufalme wa Mungu.

Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana wa pendo lake, ambaye katika yeye tunaukombozi yaani masamaha wa dhambi, Wakolosai 1;73.

2.     Katiba ya ufalme wa Mungu.

Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wane na wale wazee ishirini na wane wakaanguka mbele za mwana – kondoo, kila mmoja wao anaa kinubi na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato ambayo ni maombi ya watakatifu, Ufunuo 5;8.

 

3.     Sheria ya ufalme

Mwanangu usiisahau sheria yangu, bali moyo wako uzishike amri zangu. Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima na amani , Mithali 3;1-2

4.     Uchumi wa ufalme wa Mungu.

Nchi na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake, Zaburi 24;1.

Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu, asema Bwanawa majeshi, Hagai 1;8,

5.     Familia ya ufalme wa Mungu.

Mwili mmoja na Roho moja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. Bwana mmoja , imani moja, ubatizo mmoja, Mungu mmoja naye Baba wa wote aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote “waefeso 4;4-6.

Nami nikaanguka mbele ya miguu yake ili nimsujudie akaniambia angalia usifanye hivi mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushindi wa Yesu, Msujudie Mungu kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya  unabii, Ufunuo 19;10,

6.     Jeshi la ufalme wa Mungu

Yakobo akashika njia yake na malaika wa Mungu wakakutana naye, Naye Yakobo alipowaona alisema, Hili ni jeshi la Mungu, Akapaita mahali pale mahanaimu, Mwanzo 32;1-2

 

 

KUSUDI LA MUNGU NDANI YAKO.

Kusudi; Ni wazo au lengo lililowekwa ndani ya moyo wako ili liweze kutimiza lile ambalo Mungu ameweka katika maisha yako, watu wengi wamekuwa wakiishi katika maisha yao bila kujua kusudi alilonalo watu wanishi maisha feki

Atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa kuwa ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili mwana wa Mungu alidhihirisha ili azivunje kazi za ibilisi, 1Yohana 3;8.

Angalieni nitawapeleka  Eliya nabii , kabla haijaja siku ile ya Bwana iliyokuu na kuogofya. Naye ataigeuza mioyo  ya baba iwaelekee watoto wao na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana, Malaki 4;5-6.

Kabla sijakuumba katika tumbo nalikukujua na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa, nimekuweka kuwa nabii wa mataifa “Yeremia 4;1.

 =Kabla sijakuumba nalikujua.

Maana yake Mungu anajaribu kumwambia Yeremia kwamba natambua kabisa nilichokuwa nafanya pindi nilipokuumba.

 

=Nimekuweka juu ya mataifa na juu ya mfalme.

Maana yake kumuumba kwa kusudi lake ndani yake,

*kuwa nabii wa mataifa

*kuwa juu ya mataifa

*kuwa juu ya falme.


=Akampa na kazi ya kufanya.

*kung’oa

*kubomoa

*kuangamiza

*kuharibu

*kujenga na kupanda

Angalia nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung’oa na kubomoa na kuharibu na kuangamiza, ili kujenga na kupanda, Yeremia 1;10.

 Kuwepo kwako leo ni kwaajili ya kusudi la Mungu ndani yako. Ndani ya kusudi lako upo uwezo na mamlaka ya kuamuru na kubadilisha mazingira pinzani juu yako utakutana na falme na ngome za maadui, vita, mapepo, wachawi, utapambana navyo.

 

JINSI YA KUTAMBUA KUSUDI LAKO

Kutambua kusudi ulilo nalo ni kazi sana

Mfano: mtu anafanya biashara hii au anafanya kazi ile au anajaribu kufuga kuku, kulima lakini mtu anaona bado kuna kitu kinadaiwa anataka akifanye.

 

a.     Mungu kukuonyesha katika ndoto na maono kimsingi Mungu ndiye anayeweza kukuonyesha au kusema na wewe, kwamba wewe nani? Kwa njia ya ndoto na maono.

“kwa  kuwa Mungu hunena mara moja naam hata mara  ya pili ajapokuwa mtu hajali katika ndoto, katika maono ya usiku, usingizi mzito uwajiliapo watu katika usingizi kitandani. Ndipo huyatumia maskio ya watu na kuyatia mihuri mafundisho yao”. Ayubu

 

“Yusufu akaota ndoto akawapa ndugu zake habari nao wakazidi kumchukia, akawambia tafadhali sikieni ndoto hii niliyoita  tazama sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani kumbe mgawawangu ukaondoka ukasimama na tazama miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu. Ndugu zake wakamwambia je kweli wewe utatumiliki sisi nawe utatutawala sisi------------“. Mwanzo 37;5-8

 

“Akaota tena ndoto nyingine akawambia ndugu zake, akasema angalieni nimeota ndoto nyingine na tazama jua na mwezi na nyota kumi na moja zinaniinamia. Akamwambia baba yake na ndugu zake baba yake akamkemea akamwambia, ni ndoto gani hii uliyoita?  Je mimi na mama yakona ndugu zakotutakuja tukusujudie hata nchi?”.  Mwanzo 37:9-10

 

b.     Kiwango chako cha imani kiendane na kusudi lako (kuwa na imani nachokwa kile unachoelewa) ili uweze kujua upo ndani ya kusudi lako amani ndani ya moyo wako itakuwepo utapenda kulifafanya bilakujali mazingira yakoje. Mfano lipo jambo umewahi lifanya na tayari umekwisha kulifanya na ukasikia amani ndani ya moyo wako hata kama ni dogo tambua kuwa hilo ndilo kusudi la Mungu kwao.

“ Yusufu  akamwambia Farao ndoto ya Farao ni moja. Mungu amemwonyesha Farao atakayo yafanya hivi karibu”. Mwanzo 41:25

 

 

c.      Kupitia kwa watumishi wa Mungu na watu wengine

“Ndipo samweli akaatwa pembe yenyemafuta akamtia mafuta kati ya ndugu zake na roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa nguvu taku  siku ile---------“ 1Samweli 16:13

 

d.    Jinsi vile unavyo onekana mbele za watu

“Akamwona Petro akikota moto akamkazia macho akasema wewe nawe ulikuepo pamoja na Yule Mnazalet Yesu”. Marko 14:67

e.      Mungu kusema na wewe waziwazi  (malaika wa Mungu kukutokea)

“haya basi nitakutuma kwa Farao ili upate kuwatoa watu wangu hao wana wa Israeli katika Misri”. Kutoka 3:10

“ Malaika wa BWANA akamtokea katika mwali wa roho uliotoka katikati ya kile kijiti akatazama na kumbe kile kijiti kiliwaka  moto, nacho kijiti hakikuteketea”. Kutoka 3:2