Thursday, May 15, 2025

MASHIMO YA KICHAWI (Kiroho)

 

MASHIMO YA KICHAWI (Kiroho)

Agano la kale mtu alipokuwa anafanya kosa au makosa alikuwa anahukumiwa kwa kutupwa kwenye mashimo marefu.

Mashimo yaliyokuwepo

        i.            Mashimo yenye wanyama mfano Danieli

      ii.            Shimo lenye moto mfano Shedraka,Meshaki na Abednego

    iii.            Shimo lenye maji mengi au matope mfano Yeremia 38:6

   iv.            Shimo lisilo na kitu

Sasa

Shetani naye vile vile naye ameyaweka mashimo yake haya kwa namna ya kiroho,hayaonekani kwa macho ya kawaida kwasababu shimo lenyewe ni roho kamili,lina akili,linaweza kukimbia na ukiingia ndani huwezi kutoka linageuka na kuwa giza.Zaburi 35:7,Ufunuo 9:1-2,Isaya 24:17,14:15,Isaya 38:18

Miji inaweza kuwa na mashimo ya rohoni na utakaposhughulika na shimo hilo unakuwa umeuteka mji.Kuna mashimo makubwa  yaani kuzimu ya angani,kuzimu ya baharini ,kuzimu ya nchi

Pia kuna vishimo vidogo mfano mtu anachukuliwa msukule na kuwekwa kabatini,kisimani,dukani,n.k Isaya 42:22

Kila mtu amewekewa Baraka zake sehemu Fulani mfano kwenye kinywa,tumbo,kumbukumbu,biashara,ndoa n.k

Familia,ukoo wanawekwa kwenye mashimo ya mauti,magonjwa,laana,mikosi,shida,balaa,utasa,umasikini n.k

Mambo unayotakiwa kuyafahamu kuhusu kuzimu

         i.            Malaika wa kuzimu ufunuo 9:11

       ii.            Makomeo ya kuzimu Ayubu 17:16

     iii.            Milango ya kuzimu Ayubu 38:17,Mathayo 16:18

     iv.            Kamba za kuzimu 2Samweli 22;6

       v.            Makao ya kuzimu Zaburi 89:88

     vi.            Shida za kuzimu Zaburi 116:3

   vii.            Kitanda cha kuzimu Zaburi 139:8

Maombi

-kuyashambulia mashimo yote ya kichawi

-kuwateketeza walinzi wa mashimo

-kutoka shimoni

No comments:

Post a Comment