Tuesday, May 6, 2025

MUHIMU SANA KWA KILA MTUMISHI ALIYEONDOKA KATIKA HUDUMA NYINGINE

 MUHIMU SANA KWA KILA MTUMISHI ALIYEONDOKA KATIKA HUDUMA FULANI.

Kwanza itambulike kuwa kutoka huduma moja kwenda huduma nyingine, sio dhambi wala tatizo,tatizo linaweza kutokea katika namna ya kuondoka.

Baadhi yetu wahudumu wa injili(nikiwemo mimi) tumetokea(tulikuzwa na kulelewa) katika huduma nyingine, na sasa tupo katika huduma nyingine. Hili sio tatizo, tatizo tuliondokaje kule?

Swali la muhimu la kujiuliza kila Mtumishi wa MUNGU aliyeondoka huduma fulani, "NILIONDOKAJE KWENYE HUDUMA ILE?" Je! Niliondoka kwa dhamira njema au mbaya? Nini kilipelekea kuondoka kwangu katika huduma ile? Na maswali mengine Kama hayo kila aliyeondoka katika huduma anapaswa kuwa na majibu yake.

NDUGU MTUMISHI WA MUNGU.

Ikiwa uliondoka katika huduma fulani na moyo wako unatambua kuwa ULIONDOKA VIBAYA, na Roho Mtakatifu amekuwa akisema na wewe kuwa ULIONDOKA VIBAYA KATIKA HUDUMA FULANI, fanya haya;

1:- RUDI MBELE ZA MUNGU KWA TOBA.

Mungu ni MUNGU anayerehemu kwa kila aliyejitambua kuwa anahitaji huruma zake. MUNGU si MUNGU wa machafuko, ikiwa umeondoka kwa namna ya ouvu/ubaya...hatatembea katika ule mtembeo wake dhidi ya utumishi na huduma uliyobeba.

Msingi wa huduma yenye matokeo ni kuwa na Ushirika usiotiliwa shaka na Mungu kwanza. Tutafuteni Ufalme wa MBINGUNI kwanza na haki yake, na hayo mengine tutazidishiwa..... mafanikio tunayoyataka kwenye huduma ni mengineyo.......msingi ni MUNGU KWANZA.

2:- RUDI KWA KIONGOZI WA HUDUMA ULIYOONDOKA, MUOMBE MSAMAHA ILI MOYO WAKE UKUBARIKI.

Ni tendo la baraka kupata baraka ya kihuduma/utumishi kutoka kwa kiongozi/Mtumishi wa MUNGU ambaye aliyewekeza Imani, gharama na muda wake.

Ni hatari kutumika huku aliyefanyika Baraka ya Utumishi wako kutambulika akiwa mwenye huzuni/uchungu moyoni dhidi ya utumishi wako(wangu).....kwa sababu ya kumlipa mabaya badala ya mema.

Wahenga walisema "Muungwana akikosea, huchutama". Tutafute kwa BIDII kuwa na Amani na watu wote ....Baraka nyingine zipo mikononi mwa watu.

KUMBUKA.

1:- Kujua kupangilia masomo/mahubiri haiwezi kuwa chanzo cha kufanikiwa kihuduma......mkono wa Bwana MUNGU unahitajika zaidi.

2:- Kuna ugumu Mtumishi wa MUNGU anaweza kukutana nao kwenye Utumishi wake kwa sababu ya msingi uliojenga huduma yake.

Fikiria......!

Mtumishi wa MUNGU ambaye alikataa maonyo katika huduma fulani na akaamua kuondoka....atawezaje yeye kusikilizwa katika kuonya kwake? Imeandikwa "Mungu hadhihakiwi, apandacho mtu ndicho atakachovuna".

Kama mtu amekataa kuonywa...hana mamlaka ya kuonya wengine, na hata akiwaonya ....hatasikilizwa.

3:- Tunahitaji matamko ya viongozi wetu katika huduma ili tuweze kuvuka/kupata mpenyo zaidi.

Ni ukweli usiotiliwa shaka kuwa MUNGU ndiye huachilia mpenyo....lakini watumishi wake hiyo Neema ameichilia ndani yao. Wakitamka Neno huwa!

USIENDELEE KUPAMBANA KIHUDUMA, RUDI UKATENGENEZE ILI UENDELEE KATIKA BARAKA.

Ukiondoka mahali kwa ugomvi,vurugu na Mambo yote yasiyompendeza Bwana MUNGU.... shetani anapata uhalali wa kukushambulia. Wala usimpe nafasi ibilisi, rudi katengeneze.Katika kurudi kwako unapaswa kwanza umuulize Mungu maana wengine Ni hatari wanaweza wakakufanyia mabaya.Heshimu watu Ila usiamini watu.Wengi walipoteza maisha yao baada ya kuona Kama alikosea baadae hatari ilimpata.Ni vizuri zaidi ukatengeneza na Mungu Kama huyo mtumishi unajua alivyo.Kama anakuombea mabaya,anakuwazia mabaya na kutamka babaya juu yako mkwepe Sana,watumishi wa Mungu wengi wao Ni wivu unawasumbua na kumbuka wivu Ni uchawi.

MAOMBI YA KUOMBEA UFALME WA MUNGU NA WA SERIKALI

 πŸ“–DAY 5: MFUNGO WA MAOMBI YA SIKU 21, TAREHE 10/JANUARI/2025.


MAOMBI YA KUOMBEA UFALME:

Mathayo 6:33

Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

Ayubu 42:10

Kisha BWANA akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; BWANA naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza.

KUOMBEA UFALME NI KUWA NA MOYO WA KUPENDA KUONA WENGINE WAKISTAWI KWENYE NDOA, BIASHARA, UONGOZI NA SIASA NK.

KUOMBEA UFALME KUNATOKANA NA KUTOKUFURAHIA KUONA WENGINE WAKIHARIBIK I


MAHITAJI KWA AJILI YA KUOMBEA UFALME NA MASILAHI YA UFALME WA MUNGU:

1. MOYO SAFI, Moyo unaoshuka na kunyenyekea na kujawa na Toba na Rehema. 

MAOMBI: BABA, KTK JINA LA YESU, NAOMBA UPONYE MOYO WANGU, UPONYE MAJERAHA YOTE NA MAKWAZO YOTE, UTEKETEZE KILA UCHAFU MOYONI MWANGU KWA MOTO WA ROHO MTAKATIFU (Nena kwa Lugha, Omba kwa Roho na Uruhusu Roho Mtakatifu moyoni mwako)

BABA KTK JINA LA YESU, NINAOMBA UNISAMEHE KWA JINSI NILIVYOKUWA MCHOYO NA MBINAFSI NA HIVYO KUTOKUWAJIBIKA KWA MAHITAJI YA UFALME IPASAVYO.

Baba, Ninaomba Uniumbie kwa Upya, Moyo wa Upendo, Moyo wa Nyama, Moyo wa kufurahia kuona wengine wakistawi, Moyo wa Unyenyekevu na Toba, Moyo wa kufurahia Mafanikio ya Ufalme na Wana wa Mungu.

BAADA YA KUOMBA MAOMBI HAYA YA UFALME HAKIKISHA UNAFURAHIA KUONA WENGINE WANAINUKA NA KUINULIWA. (Usifurahie kuona Wana wa Mungu Wanaharibikiwa, Wanakwama nk)

Mfano: Ukisikia Ndugu/Rafiki Ameteuliwa na Raisi kushika Cheo Fulani, Usione wivu,

 Ukisikia Ndugu/Rafiki amepata Tenda ya kazi ya Mabilioni Usiumie Moyo, Sherekea kuwa Mungu anawastawisha Watoto wake kwa Namna Tofauti na kwa majira totofauti

 KUOMBEA NDOA NA FAMILIA:

1. Baba, ninaomba ustawishe Kiungu NDOA na Familia za Wana wa Mungu ktk Jina La Yesu.

2. Baba, Ninamuombea kila Binti na Kijana Anayehitaji Ndoa , Umbariki na Ndoa Nzuri mwaka huu katika Jina La Yesu.

3. Baba, Ninaombea kila Ndoa Inayopitia Changamoto ya Migogoro, Uitulize na kuihuisha katika Jina La Yesu.

MAOMBI YA KUOMBEA UCHUMI, BIASHARA NA UWEKEZAJI

BABA, KTK JINA LA YESU, NINAOMBA UMSTAWISHE KIUNGU KILA MWANA WA MUNGU KWENYE UCHUMI, BIASHARA NA UWEKEZAJI WAKE KTK JINA LA YESU.

 BABA, NINAOMBEA KILA MWANA WA MUNGU MWENYE KITEGA UCHUMI, KAMPUNI, KIWANDA, DUKA, SHAMBA NA MRADI WOWOTE, MWAKA HUU, UMFANYIE MIPENYO YA FAIDA MARADUFU KTK JINA LA YESU.

 BABA, NINAMUOMBEA KILA MWANA WA MUNGU ANAYETESWA NA MADENI KWENYE BIASHARA ZAKE NA UWEKEZAJI, BWANA UMFANYIE MUUJIZA UTAKAOMTOA KWENYE MADENI MILELE KTK JINA LA YESU.

 Baba, ninamuombea kila Mwana wa Mwenye Malengo ya kuanzisha Biashara Mpya, Kufungua Kampuni, kujenga Kiwanda, kuanzisha miradi ya Biashara yoyote mwaka huu, Bwana Umfanyie Muujiza  wa Mipenyo ya kupata Mtaji ktk Jina La Yesu.

Baba, Ninamuombea kila Mwana wa Mungu, Kujenga Nidhamu na Mwenendo utakaomwezesha kukua kiuchumi na kudumu kustawi bila kushuka hasa kwa Uaminifu wa kulipa Fungu la kumi na kutoa Dhabihu mbalimbali za kuinua Ufalme ktk Jina La Yesu.

BABA, NINAOMBA UMWEZESHE KILA MWANA WA MUNGU KUJIHUSISHA KIKAMILIFU KWA MAMBO YA UFALME NA KUTOA DHABIHU NA RASILIMALI ZA KUINUA UFALME KTK JINA LA YESU


ENEO LA SIASA NA UONGOZI. (OMBEA USTAWI WA KITAIFA)

1. Baba, ktk Jina La Yesu Tunaombea haki na Amani kutawala Taifa letu.

2. Baba, Tunaomba Ulivushe salama Taifa letu kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu ktk Jina La Yesu.

3. Baba, Naomba Kiinuke kizazi cha Wana wa Mungu kitakachochukua Nafasi mbalimbali za Uongozi na Utawala kwenye Taifa letu ( Wana wa Mungu Wainuke sasa nal kugombea nafasi za Udiwani, Ubunge na Uraisi ktk Jina La Yesu) Wana wa Mungu Wakalishwe kwenye nafasi mbalimbali za Utawalal na Uongozi.

4. Baba, ninaomba ninaomba Waamshwe Usingizini Wana wa Mungu wpanaPaswa kuwa Waokozi wa Taifa letu, Waanze kukaa kwenye viti na Meza za maamuzi ya Utawala na Uongozi wa Nchi yetu ktk Jina La Yesu.

5. Baba, NinaAmuru kuwa Washirikina Watu wa Giza Walio kwenye Utawala na Uongozi, sasa Muhula wao na Ukomeshwe ktk Jina La Yesu, Ninaamuru wasirudi tena kwenye Uongozi na Utawala wa Taifa hili ktk Jina La Yesu.

BABA, NINAOMBA UINUE KIZAZI CHA WAOKOZI KWENYE TAIFA LETU KWENYE KILA ENEO IWE BIASHARA NA UWEKEZAJI, TAALUMA, SIASA NA UONGOZI NA IVYO KUKOMESHA KABISHA UTAWALA WA WAOVU NA WASHIRIKINA KTK JINA LA YESU. Baba, Ninaomba Ukomeshe Utawala wa dhuluma, Rushwa na Wizi wa Mali za Taifa letu kwenye Mwaka huu wa Uchaguzi ktk Jina La Yesu.

Omba kwa Imani

Omba kwa Roho

Omba ukiwa na Matarajio ya kuona Ulichokiomba kikiwa Ushuhuda machoni pako.

KUOMBA MAOMBI YA SHUKRANII


KUOMBA MAOMBI YA SHUKRANI.

Zaburi 92 : 1

Ni neno jema kumshukuru Bwana, Na kuliimbia jina lako, Ee Uliye juu.

 Yeremia 30:19

Humo zitatoka nyimbo za shukrani na sauti za wale wanaosherehekea. Nitawaongeza na wala hawatakuwa wachache; nitawafanya waheshimiwe wala hawatadharauliwa.

Yeremia 30:19

1. Mshukuru kwa ajili ya Pumzi ya Uhai na Afya.

2. Mshukuru Mungu kwa ajili ya Ulinzi na kukuepusha na Kila Uovu wa adui shetani na mabaya yote.

3. Mshukuru kwa ajili Ugavi na riziki kwa hatima yako, Family, huduma, Uzao nk.

4. Mshukuru Mungu kwa baraka zote za mwaka 2025 juu ya maisha yako, huduma, kanisa.

5. Mshukuru Mungu kwa ajili ya kukuvusha Salama toka 2024 kuingia 2025

6. Baba Asante kwa ajili ya Wokovu wa Nafsi na Injili kuhubiriwa kwa mwaka 2024

7. Baba Asante kwa Wate Uliowaleta kanisani na kuwafanya washirika na Wanafamilia.

8. Baba Asante kwa ajili ya Uwepo wako tuliofurahia kwenye Ibada zetu zote mwaka 2024

9. Baba Asante kwa ajili ya Neno la kutupatia Urithi wetu uliloliachilia kwenye Ibada zetu mwaka 2024.

10. Baba Asante kwa ajili ya Hekima na Neema ya kuwajibika uliyoiachilia juu ya viongozi wetu wa kanisa, Baba Askofu, Wachungaji, Watendakazi mbalimbali.

11. Baba, Asante kwa ajili ya Msaada wako, Neema yako na Mkono wako vilivyofanikisha Kanisa 2024.

12. Baba Asante kwa ajili ya Ustawi wa Mchungaji wetu, Pastor Baraka, mkewe na Watoto, asante kwa ajili ya Neema ya Utumishi na huduma juu yake.

13. Baba Asante kwa ajili ya Shuhuda Zote Ulizotubarikia kwa Mwaka 2024 kama kanisa na Mtu mmoja mmoja kwenye Ndoa, Uchumi, Ajira, masomo, Uzao na Kumiliki na Kuongezeka

KILA OMBI TUMIA WALAU DAKIKA 5 NA KUENDELEA,

HUSISHA KUOMBA KWA ROHO NA KUNENA KWA LUGHA.

USISAHAU KUABUDU KABLA HUJAANZA KUOMBA.

NOTE:

UKIWA KAZINI, OFISINI, TUMIA HEKIMA YA KUTOKUATHIRI KAZI, WAWEZA KUOMBA KIMOYOMOYO HUKU UKIENDELEA NA KAZI YA KUHUDUMIA, Lakini mda wa breki au Lunch jifungie mahali na Uombe.

UNABII HUU HAPA KWAKO KWA MWAKA 2025

 UNABII KWA MWAKA 2025

1. 2025 NI MWAKA WENYE NURU KILA ENEO LA MAISHA. Iwe biashara na Uwekezaji,  Siasa na Uongozi ata Taaluma, Ndoa na Familia,  Tutafufurahia Nuru ya Kiungu na hakuna kubahatisha wala kupapasa ktk Jina Yesu.  πŸ“–“Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.

  — Zaburi 119:105 (Biblia Takatifu)

2. 2025 NI MWAKA WA KUCHUKUA HATUA ZA UHAKIKA KILA ENEO LA MAISHA. HAKIKISHA UNACHUKUA HATUA KTK ENEO LAKO LA HATIMA NA HAKIKA UTAFANIKIWA KTK JINA LA YESU. πŸ“–“Uendapo, hatua zako hazitadhiikika, Wala ukipiga mbio hutajikwaa.

  — Mithali 4:12 (Biblia Takatifu) 

πŸ“–“Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake. Hatua zake hazitelezi.

  — Zaburi 37:31 (Biblia Takatifu)

3. 2025 KILA MWANA WA MUNGU ANAGEUZWA KUWA MWOKOZI KWA JAMII YAKE KWENYE ENEO LAKE, kupitia Biashara,  huduma ata siasa na Uongozi. πŸ“–Obadia 1 (Biblia Takatifu)

¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯

¹⁷ Bali katika mlima Sayuni watakuwako wenye kuokoka, nao utakuwa mtakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki milki zao.

²¹ Tena waokozi watakwea juu ya mlima Sayuni ili kuuhukumu mlima wa Esau; na huo ufalme utakuwa ni mali ya Bwana.

4. 2025 NI MWAKA WA KUFURAHIA KIBALI CHA KIUNGU KILA MAHALI UTAKAPOBISHA HODI NA KUCHUKUA HATUA. Iwe huduma, biashara na kila eneo KTK Jina La Yesu.  πŸ“–“Basi Mungu alimjalia Danielii kupata kibali na huruma machoni pa huyo mkuu wa matowashi.

  — Danieli 1:9 (Biblia Takatifu)

5. 2025 NI MWAKA WA KUFURAHIA SHUHUDA NYINGI MPYA NA ZA KUONEKANA KWA WANA WA MUNGU WATAKAO TUMIA IMANI KUTHUBUTU NA KUCHUKUA HATUA. πŸ“–“Nimeambatana na shuhuda zako, Ee Bwana, usiniaibishe.

  — Zaburi 119:31 (Biblia Takatifu)

6. 2025 KILA MWANA WA MUNGU ATAFURAHIA KUSAIDIWA NA MKONO WA BWANA KULITIMIZA KUSUDI LA KUISHI KWAKE NA KUSUDI LA HATIMA YAKE. πŸ“–“Kisha Bwana akawapa raha pande zote, sawasawa na hayo yote aliyokuwa amewaapia baba zao; wala katika adui zao wote hakusimama hata mtu mmoja miongoni mwao mbele zao; yeye Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.

  — Yoshua 21:44 (Biblia Takatifu)

7. 2025 KILA MWANA WA MUNGU AMEPEWA KUMILIKI MARADUFU NA KUONGEZEKA KILA ENEO NA KUWA NA UTAWALA. “maana nchi hii yote uionayo, nitakupa wewe na uzao wako hata milele.

  — Mwanzo 13:15 (Biblia Takatifu)

8. 2025 NI MWAKA WA KUFURAHIA AFYA YA KIUNGU KWA KILA MWANA WA MUNGU, KULINDWA NA KUEPUSHWA NA KILA UOVU KTK JINA LA YESU.  Kumbukumbu la Torati 11 (Biblia Takatifu)

¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯

¹¹ lakini nchi mwivukiayo kuimiliki ni nchi ya vilima na mabonde, nayo hunyweshwa maji ya mvua ya mbinguni;

¹² nayo ni nchi itunzwayo na Bwana, Mungu wako; macho ya Bwana Mungu wako, ya juu yake, tangu mwanzo wa mwaka hata mwisho wa mwaka.

9. 2025 NI MWAKA WA KUFURAHIA KASI YA KIMUNGU KWENYE KULITIMIZA KUSUDI NAHAKUNA KUCHELEWESHWA KTK JINA LA YESU.  πŸ“–“Basi uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Maneno yangu hayatakawilishwa tena hata moja, bali neno nitakalolinena litatimizwa, asema Bwana MUNGU.

  — Ezekieli 12:28 (Biblia Takatifu)

10. KILA MWANA WA MUNGU ATAFURAHIA NEEMA YA KUSTAWISHWA PANDE ZOTE, KUSTAWISHWA NA KUSTAREHESHWA KILA ENEO LA MAISHA NA KUSUDI LA KUISHI.  Tutafurahia kuvuka vizuizi na kushinda Upinzani,  tutavuka mipaka ya kiroho na kiuchumi.  Kupanda Kiwango mwaka huu ni urithi wa kila mwana wa Mungu. Ni pamoja na kurejeshewa kila chema alichotuibia adui ktk Jina La Yesu. 

 πŸ“–“Na Yuda wote wakakifurahia kile kiapo; kwani wameapa ............ ; naye Bwana akawastarehesha pande zote.

  — 2 Mambo ya Nyakati 15:15 (Biblia Takatifu).

NA HAKIKA NDIVYO ITAKAVYOVYOKUWA KTK JINA LA YESU,

ZIJUE SABABU ZA KUMILIKI COINS

 `Zijue Sababu 10 za Kumiliki Asset Coins (yaani, sarafu za kidijitali zenye thamani halisi au zinazoungwa mkono na mali fulani kama dhahabu, ardhi, au mali za kampuni) kunaweza kuwa na manufaa mengi. Sababu 10 kwanini unaweza kufikiria kumiliki Asset Coins:

1. Ulinzi dhidi ya mfumuko wa bei: Asset coins kama zile zinazoungwa mkono na dhahabu zinaweza kusaidia kuhifadhi thamani ya fedha zako wakati wa mfumuko wa bei.

2. Urahisi wa upatikanaji wa mali: Zinakupa fursa ya kuwekeza kwenye mali kubwa (kama dhahabu au ardhi) kwa kiasi kidogo cha pesa.

3. Uwazi na ufuatiliaji: Teknolojia ya blockchain inawezesha uwazi wa miamala, hivyo unajua thamani yako iko wapi na inafanyiwa nini.

4. Uwekezaji wa kimataifa: Asset coins hukuwezesha kuwekeza kimataifa bila kuhitaji kuwa na akaunti za kigeni au kupitia mchakato wa kisheria wa nchi husika.

5. Uhamishaji wa haraka na rahisi: Unaweza kuhamisha thamani (asset coins) kwenda kwa mtu mwingine popote duniani haraka na kwa gharama ndogo.

6. Mapato ya ziada: Baadhi ya Asset Coins Mfano $MLC $BNB nk.. hukupa faida ya ziada kupitia staking au riba ya uwekezaji.

7. Ulinzi wa mali: Ni njia ya kuhifadhi mali zako kwa usalama, hasa katika maeneo yenye changamoto za kiuchumi au kisiasa.

8. Tofauti ya uwekezaji (diversification): Inakusaidia kupanua mseto wa uwekezaji (diversify portfolio) na kupunguza hatari ya kupoteza fedha zote.

9. Uwezekano wa ukuaji wa thamani: Kama mali inayounga mkono sarafu hiyo inaongezeka thamani, basi na Asset Coin yako inaongezeka pia. Buy assets buy MLC. 

10. Kujihusisha na teknolojia mpya: Inakupa nafasi ya kuwa sehemu ya mapinduzi ya kidijitali na kifedha ambayo yanaathiri dunia nzima.

FUNDAMENTAL CRYPTO ANALYSIS

*FUNDAMENTAL ANALYSIS (FA)*

Fundamental Analysis ni mbinu ya kuchambua thamani halisi ya mali ya kifedha kwa kuchunguza mambo ya msingi yanayoathiri bei yake. Katika ulimwengu wa cryptocurrency, FA inalenga kuchambua vigezo kama:

*Utility ya Tokeni* – Je, tokeni ina matumizi halisi katika mfumo wake wa ikolojia?

*Team na Maendeleo* – Je, timu ya mradi ina uzoefu na uwezo wa kutekeleza maono yao?

*Tokenomics* – Ugavi wa tokeni, namna zinavyogawiwa, na mpango wa kuchoma (burning mechanism).

πŸ‘‰ *Total Supply* 
Hii ni Jumla au idadi ya coin au Token zotee ambazo ziko kwenye Ecosystem.

πŸ‘‰ *Circulating Supply*
Hi ni Jumla au idadi ya Coin au Token zote kwenye Ecosystem ambazo zinakuwa zimeshaingia kwenye mzunguko au sokon.

πŸ‘‰ *Volume Supply*
Hii ni Jumla ya miamala yote ambayo imeshafanyika kwenye coin au Token Husika ndani ya masaa 24.

πŸ‘‰ *Market cap*
Hii ni Jumla ya Mtaji wote ambao upo kwenye coin au Token ambazo ziko kwenye mzunguko.

NB:πŸ‘‰Circulating supply ukiizidisha na Currency price ya Coin Husika ndiyo unapata Market cap.

*Community Strength* – Ushirikiano na ukuaji wa jamii inayounga mkono mradi.

*Partnerships & Integrations* – Je, mradi unaushirikiano gani wa kimkakati?

*Roadmap* – Mpango wa maendeleo wa mradi ukoje na je, wanafuata mipango yao?

*White paper* - White Paper ni hati rasmi ya kiufundi na kibiashara inayotoa maelezo ya kina kuhusu mradi wa sarafu ya kidijitali (cryptocurrency). Hati hii hutumika kueleza matatizo yanayolengwa kutatuliwa na mradi husika, suluhisho linalopendekezwa, teknolojia inayotumika, pamoja na maelezo ya kiuchumi kama vile tokenomics, usambazaji wa tokeni, na mpango wa maendeleo (roadmap).

*Umuhimu wa White Paper katika Mradi wa Cryptocurrency*

1. Kuaminika kwa Mradi:
White paper huonyesha uwazi na dhamira ya waandaaji wa mradi, hivyo kuongeza uaminifu kwa wawekezaji na jamii ya crypto.

2. Kutoa Maarifa kwa Wawekezaji:
Inawawezesha wawekezaji kuelewa thamani ya mradi, malengo, na nafasi yake katika soko kabla ya kuwekeza.

3. Mwongozo wa Maendeleo:
White paper ni dira ya kiufundi na kimkakati inayowaongoza watengenezaji wa mradi katika kutekeleza hatua kwa hatua kulingana na roadmap.

4. Kuvutia Ushirikiano na Rasilimali:
Wawekezaji wa taasisi, washirika wa kiteknolojia na jumuiya hupima ubora wa white paper kabla ya kujiunga au kuwekeza katika mradi.

5. Msingi wa Tokenomics:
Inafafanua kuhusu usambazaji wa tokeni, bei ya awali, matumizi ya fedha zilizokusanywa (fund allocation), na modeli ya uchumi wa tokeni.

Mfano:
Bitcoin white paper (iliyotolewa na Satoshi Nakamoto mwaka 2008) ndiyo msingi ulioanzisha mapinduzi ya fedha za kidijitali. Vivyo hivyo, kila mradi mpya unaotaka kuaminika lazima uandike na kuchapisha white paper yenye maudhui sahihi na ya kuvutia.

Hivyo Lengo kuu la Fundamental Analysis(FA):
Kupata picha halisi ya thamani ya tokeni kwa misingi ya kiuchumi, teknolojia, na mwenendo wa soko ili kusaidia wawekezaji kufanya maamuzi sahihi ya muda mrefu.

Thursday, May 1, 2025

MAJINA YALIYOANDIKWA KWENYE KITABU

 

MAJINA YALIYOANDIKWA KWENYE KITABU

Kuna  aina mbalimbali za vitabu

-vitabu vya kiroho

-vitabu vya kimwili

Na kila kitabu kinalenga kutoa maarifa kwa mtu,Mathayo 1:1---kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo.Wafilipi 4:3,kitabu cha uzima,Ufunuo 3:5-6,Ufunuo 13:8,Ufunuo 20:12

JE,ATAKUPA RUHUSA?

Ruhusa ni ombi linalofanywa na watu wawili au kikundi cha watu ili muende mahali Fulani.Katika kuomba ruhusa kuna mambo mawili,ukubaliwe au ukataliwe Kutoka 5:1----nyoka,damu,vyura,chawa,mainzi,tauni,majipu,mvua yam awe na moto,nzige,giza

 

KIPOFU TANGU KUZALIWA

Kipofu:Ni mtu asiyeweza kuona/ni mtu asiyejua siri za ufalme wa mbinguni.Yohana 9:1-41 Bethaida,Marko 10:46-52 Yeriko-Bartimayo,2Petro 1:9------

 

MAUTI ILIYOPANDWA KWENYE ARDHI

Ardhi-nchi-inamipaka halali ya umiliki Mwanzo 3:17-18

·        Ardhi inasikia,ardhi ina masikio Yeremia 22:29

·        Ardhi inakinywa,Ufunuo 12:15-17,Mwanzo 4:12

·        Ardhi ni store,kuna ardhi zimeandikiwa habari chafu,mbaya n.k 2Nyakati 7:14-18

 

HATA WAKUSEME,SONGA MBELE

1Samweli 17:23,Mwanzo 37:18---,Kutoka 2:13---,Kutoka 14:15----,Zaburi 124:1-----Mathayo 27:39

 

NGUVU YA UFUFUO

Nguvu ni uweza wa kutenda jambo Fulani isivyo kawaida

Ufunuo kukomboa/kuvunja,Luka 20:36,Isaya 26:19,Yohana 11:25----,Ezekieli 37:1-10

 

MALIKIA WA BAHARI

Ni pepo anayetawala dunia kwenye Nyanja zote,kwenye ndoa,uchumi.Anatawala mashariki,kaskazini,magharibi,kusini,Na kwenye anga kuna mkuu wa pepo,huyu pepo malkia wa bahari ni mungu mke kule Efeso walikuwa wanamwita atemi,Matendo 19:27,1Wafalme 11:33

Kazi anazozitenda

·        Anashikilia anasa zote

·        Anashikilia fedha za dunia

·        Ni pepo la uharbifu

·        Anatawala kwenye maji

·        Linazuia maombi Danieli 10:13

·        Hasira za kupitiliza

·        Kuwekea vitu moyoni

Ufunuo 17:1-18

 

KINYWA CHAKO ATAKIJAZA KICHEKO

Kicheko:ni namna ya kupata furaha kwa mtu,lakini kicheko hicho kinaweza kuwa kibaya au kizuri ila hapa nazungumzia kicheko kizuri cha furaha cha habari njema,Ayubu 8:19-22,Zaburi 126:2,Mwanzo 21:5-7

 

KUHARIBU MIZIMU YA UKOO

Mizimu ni mashetani wanaoendana na mila na desturi za jamii.wachawi wanajuana kutokana na mizimu katika shughuli zako Kutoka 23:32-33,Isaya 8:19,torati 18:10-12

 

RATIBA ZA KISHETANI

Ni utaratibu uliowekwa kwa ajili ya jambo Fulani.Utaratibu huo unawekwa kwa lengo na makusudi Fulani kwa kufuata hatua baada ya hatua.Waamuzi 13:2-5,Waamuzi 13:24,Waamuzi 16:1-3,Waamuzi 16:4---

Yuda,Othnieli,Ehudi,Deborah,Gideoni,Tola,Yairi,Yefta

 

MOYO ULIOJERUHIWA

Moyo kujeruhiwa unatokana na sababu mbalimbali mfano kuachwa,kupigwa,kusalitiwa n.k Mithali 15:13-15 moyo uliyojeruhiwa mtu anakuwa na hasira sana na ugomvi Mithali 15:18,Mithali 15;28,Mithali 15:1,Mithali 16:1

 

MASHAMBA YA KIROHO

Shamba ni sehemu inayotumika kupanda mbegu

Luka 8:5-8

        i.            Njia

      ii.            Mwamba

    iii.            Miiba

   iv.            Udongo mzuri

-Mpanzi ni mtumishi wa Mungu

-Shamba ni moyo

-Mbegu ni Neno la Mungu

Luka 8:11-15,1Wakorinko 3:8-9

MASHAMBA YA KIROHO

 

MASHAMBA YA KIROHO

Shamba ni sehemu inayotumika kupandia mbegu.Kiroho shamba ni moyo na mbegu ni Neno la Mungu Mathayo 13:3-,Luka 8:1----

 

UTUPE LEO RIZIKI YETU

Riziki maana yake ni Baraka,mafanikio,mali,afya,fedha n.k

Mathayo 6:9-11,Mathayo 7:7-11,hagai 2:8,

3Yohana 1:2,Isaya 45:1-6

NEEMA YA KUOMBA ALFAJIRI NA ASUBUHI

Zaburi 5:1-3

Ni maombi ya mamlaka ya kuharibu mipango ya kishetani iliyofanyika juu yako.

Ni maombi yenye uweza wa kupata Baraka na kibali

 

ALIYEFUNGWA

·        Kifungo ni hali ya kuwa utumwani

·        Ni hali ya kuwa kwenye mateso

·        Ni hali ya kuwa kwenye shida

·        Ni hali ya kutokuwa huru

·        Ni kupindishwa/kuzuiwa

Marko 11:1-11

Luka 19:29-40

Mathayo 21:1-11

Luka 14:1-6

Hesabu 22:22---------

Baraki anabariki na kulaani

 

MWEZI WA KUKUTANA NA MUNGU

Namba sita kibiblia ni namba ya mwanadamu

Mwanzo 1:26-31

Ezekieli 8:1-4

Hagai 1:14-15

Luka 1:26

TANZI ZA MAUTI

Mithali 13:14

Mithali 14:27

2Wafalme 4:40,Ayubu 5:20,Zaburi 49:14,Zaburi 68:20,Mathayo 4:16,2Wakorintho 2:15-16

 

KISIWA CHA MATESO

Kisiwa ni eneo la nchi kavu katikati ya bahari,ziwa au mto linalozungukwa na maji. Ufunuo 1:9,Ufunuo 16:20,matendo 28:7,Matendo 28:9

Yohana-alitumbukizwa kwenye pipa la mafuta yaliyokuwa yanachemka,aliwekwa kwenye gereza la migodi kisiwa cha Patimo (Uturuki)

 

AGANO LA KITOVU

Agano ni mkataba au makubaliano kati ya watu wawili au zaidi,kati ya pande mbili.Kuna agano la Kimungu na agano la kishetani.Shida unayopitia ni kutakana na agano lililofanyika juu yako kupitia kitovu ulipozaliwa kuna jambo lilifanyika. Zaburi 71:6-sala /maombi ya Daudi.Ezekieli 16:1-5,1Wafalme 18:17-19

 

MGONGANO WA FALME MBILI

Mathayo 4:23----

Isaya 5:14-15

UMWINUA MNYONGE

1Samweli 2:8,Torati 17:17,1Wafalme 11:1-----

 

ATAAGIZA MALAIKA WAKULINDE

Zaburi 91:10------

Zaburi 35:1-7

 

ULIANZA MWENYE HUZUNI

1Nyakati 4:9-10

Danieli 6:3-4

Danieli 3:28

 

WAKUACHE UONEKANE

Wafilipi 3:9-10

1Samweli 16:1-17

 

 

KUZIKOMBOA SEHEMU ZA MTU

 

KUZIKOMBOA SEHEMU ZA MTU

-Roho

-Nafsi

Mwili

Kikawaida ili mtu aweze kuharibikiwa au asifanikiwe,shetani huwa anashughulika na sehemu hizo,ili kuleta uharibifu

1.     Mji wa Mafanikio

Hapa tunazungumzia mali,fedha,uchumi mzuri,utajiri,maisha mazuri n.k

Torati 28:1-13

Hapa ni sawa na kusema password za maisha

2.     Mji wa Afya

Hapa tunazungumzia afya njema,uhai,kuishi

3Yohana 1:2,Mithali 3:7-8,Isaya 58:8,Yeremia 30:17,33:6.

Shetani akipachezea ndiyo mtu anakuwa mgonjwa,mauti,kifo,maumivu n.k

3.     Mji wa Mahusiano

Hapa tunazungumzia Mungu,urafiki,undugu,upendo.Shetani akipachezea hapa,chuki itatengenezwa hapa,unaweza kumuona mke/mumeo kawaida tu.1Samweli 18:1-5,Waamuzi 19:3,Yohana 15:13

4.     Mji wa Kumbukumbu

Hapa hunazungumzia akili,ufahamu,maarifa,kuelewa,kuyashika unayofundishwa.Hapa pakichezewa utaona mtu amejiua,amechanganyikiwa,kusahausahau n.k

5.     Mji wa Sheria

Hapa tunazungumzia kanuni,taratibu,hiyali ya mtu,amri,hekima,adabu,heshima,maadiki.Mithali 3:1

Hapa wizi ndio unapoanza kwa mtu kama pakiharibiwa

6.     Mji wa Ndoto

Hapa tunazungumzia uwezo wa kutafsiri ndoto,kuota,macho ya rohoni-kufunguka jicho la tatu.Danieli 5:12

7.     Mji wa Vita

Hapa tunazungumzia ulinzi,vita vya rohoni,maombi,mashambulizi,nguvu za kiroho

Hapa ndiyo kituo cha pepoau jinni Torati 20:19-20,Hesabu 21:14,waefeso 6:10-12

KUBOMOA TAWALA ZA KISHETANI

 

KUBOMOA TAWALA ZA KISHETANI

Mamlaka ni utawala,nguvu,amri,jeshi,fedha

Serikali-Ikulu,Bunge, na mahakama

1.Mkuu wa anga

Huyu ni shetani anayekaa na kutawala kwenye anga kwa ajili ya kuzuia maombi Danieli 10:11-13

2.Mkuu wa ardhi

Huyu ni shetani anayesimamia kuharibu ardhi

Ufunuo 9:11

Ufunuo 13:11

Mkuu wa bahari

Huyu ni shetani anayetawala maeneo yote yanayohusioana na maji na ndiye anayesimamia

Ufunuo 13:1

 

KILA ULIMI ULIOINUKA JUU YAKO

Ulimi ni kiungo kimoja wapo ndani ya mtu,wanyama na viumbe vingine

Isaya 54:17

Zaburi 10:7

Mithali 12:18

Mithali 15:4

Mithali 18:20-20

Yakobo 1:26

 

KUIKOMBOA NAFSI

Mtu ana sehemu tatu

       i.            Roho (spirit)

     ii.            Nafsi (soul)

  iii.            Mwili (body)

1Wathesalonike 5:23

1Wakoritho 15:44-49

Kazi ya nafsi ni kuunganisha mwili na roho

Roho:Inahusisha mambo ya Mungu

·        Maombi (ibada)

·        Ushirika na Mungu

·        Vita vya Kiroho

·        Ndoto

·        Dhamiri (kupambanua)

·        Shuhuda kwa watu

Nafsi:Kigiriki maana yake ni kiumbe kilicho hai.Kiebrania maana yake ni kile kinachopumua.Nafsi ni ile sehemu ambayo ina ufahamu wa mtu mwenyewe

Kazi yake

·        Hisia,tama,upendo

·        Utashi,nia,kuamua

·        Kufikiri,kutafakari,kuona

Mwili:unahusika na mambo ya ulimwengu

 

MSHAURI WA AJABU

Mshauri:Ni mtu anayetoa maelekezo kuhusu kutengeneza jambo Fulani/ni mapendekezo kuhusiana na jambo Fulani Warumi 11:33-36,Isaya 9:6

 

BARAKA ZA ROHONI

Baraka:Ni mafanikio juu ya mtu.Mambo yote unayoyaona ulimwengu wa mwili yanaanzia ulimwengu war oho kwasababu sisi ni roho pia ni mwili Waefeso 1:3------

VUKA

Ni kitendo cha kushinda kukwepa vikwazo/ni kitendo cha kwenda upande wa pili yaani ng’ambo

Matendo 16:9-11

Luka 8:22-------------

 

MBEGU MBAYA ILIYOPANDWA

Mbegu ni chanzo cha uhai

Aina za mbegu

-mbegu njema (Neno la Mungu)

-mbegu mbaya (Neno la shetani)

Kwanini mbegu ni chanzo cha uhai? Ufalme wa mbinguni unaanza na mbegu Mathayo 13:24-30,Mathayo 13:36------

·        Mbegu njema ni Mwana wa Adamu

·        Lile konde ni ulimwengu (shamba)

·        Mbegu njema ni wana wa ufalme

·        Magugu ni wana wa Yule mwovu

·        Aliyepanda magugu ni ibilisi (shetani)

·        Wavunao ni malaika

·        Mavuno ni mwisho wa dunia

·        Ghalani ni uzima wa milele

Ufunuo 14:14-18

KIFUNGO CHA UCHUMI

 KIFUNGO CHA UCHUMI

Kifungo cha uchumi kinatokana na madhabahu za ukoo au miungu ya ukoo

Kutoka 20:1-3

Kutoka 20:4-6

Mwanzo 12:2-3

Mwanzo 32:24

Hagai 2:6-8

Mithali 8:18-21

3Yohana 1:2

NAPANDA MBEGU YA MAFANIKIO

 

NAPANDA MBEGU YA MAFANIKIO

Kitu chochote chenye uhai asili yake ni mbegu,mfano mparachichi au mwembe,n.k mbegu ninayozungumzia hapa ni mafanikio ya mtu

Mwanzo 26:12-14

Mwanzo 26:15-17

Mwanzo 26:18-19

Mwanzo 26:20-21

Mbegu inawezwa kuzuiwa au kukwama,kukwamishwa

Yoeli 1:17

Mwanzo 2:4-6

 

NGUVU YA KUITA

Kuita:ni kitendo cha kuhamuru kile unachokitaka kitokee au kije kwako

v Uhusiano wa mtu na mtu unaanzia kwenye mawasiliano

v Tunapoomba mara kwa mara tunaweka mahusiano yetu na Mungu yawe ya karibu.Na ni tofauti na mtu ambaye haombi (asiyeomba) Mwanzo 3:20,Mwanzo 16:13,Mwanzo 17:5-7,15, Mwanzo 28:12----,2Wafalme 20:1-5

v Ezekia aliamini maombi yanaweza kubadili maamuzi ya Mungu,maamuzi ya bosi wako,mumeo,mkeo,watawala,matamko ya laana,magonjwa

v Kuita kunafungua milango iliyofungwa,Yesu alimwita Lazaro.Isaya 62:6-7

v Kuita ni kutawala (kibali) Zaburi `19:14,Isaya 57:19,Mhubiri 8:4

v Kiashiria Mungu anachotumia ni kuita Zaburi 138:3,1Samweli 3:1-11,2:1-10,Isaya 42:6-7

MAJINA YALIYOANDIKWA KWENYE KITABU

 

MAJINA YALIYOANDIKWA KWENYE KITABU

Kuna  aina mbalimbali za vitabu

-vitabu vya kiroho

-vitabu vya kimwili

Na kila kitabu kinalenga kutoa maarifa kwa mtu,Mathayo 1:1---kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo.Wafilipi 4:3,kitabu cha uzima,Ufunuo 3:5-6,Ufunuo 13:8,Ufunuo 20:12

JE,ATAKUPA RUHUSA?

Ruhusa ni ombi linalofanywa na watu wawili au kikundi cha watu ili muende mahali Fulani.Katika kuomba ruhusa kuna mambo mawili,ukubaliwe au ukataliwe Kutoka 5:1----nyoka,damu,vyura,chawa,mainzi,tauni,majipu,mvua yam awe na moto,nzige,giza

 

KIPOFU TANGU KUZALIWA

Kipofu:Ni mtu asiyeweza kuona/ni mtu asiyejua siri za ufalme wa mbinguni.Yohana 9:1-41 Bethaida,Marko 10:46-52 Yeriko-Bartimayo,2Petro 1:9------

 

MAUTI ILIYOPANDWA KWENYE ARDHI

Ardhi-nchi-inamipaka halali ya umiliki Mwanzo 3:17-18

·        Ardhi inasikia,ardhi ina masikio Yeremia 22:29

·        Ardhi inakinywa,Ufunuo 12:15-17,Mwanzo 4:12

·        Ardhi ni store,kuna ardhi zimeandikiwa habari chafu,mbaya n.k 2Nyakati 7:14-18

 

HATA WAKUSEME,SONGA MBELE

1Samweli 17:23,Mwanzo 37:18---,Kutoka 2:13---,Kutoka 14:15----,Zaburi 124:1-----Mathayo 27:39

 

NGUVU YA UFUFUO

Nguvu ni uweza wa kutenda jambo Fulani isivyo kawaida

Ufunuo kukomboa/kuvunja,Luka 20:36,Isaya 26:19,Yohana 11:25----,Ezekieli 37:1-10

 

MALIKIA WA BAHARI

Ni pepo anayetawala dunia kwenye Nyanja zote,kwenye ndoa,uchumi.Anatawala mashariki,kaskazini,magharibi,kusini,Na kwenye anga kuna mkuu wa pepo,huyu pepo malkia wa bahari ni mungu mke kule Efeso walikuwa wanamwita atemi,Matendo 19:27,1Wafalme 11:33

Kazi anazozitenda

·        Anashikilia anasa zote

·        Anashikilia fedha za dunia

·        Ni pepo la uharbifu

·        Anatawala kwenye maji

·        Linazuia maombi Danieli 10:13

·        Hasira za kupitiliza

·        Kuwekea vitu moyoni

Ufunuo 17:1-18

 

KINYWA CHAKO ATAKIJAZA KICHEKO

Kicheko:ni namna ya kupata furaha kwa mtu,lakini kicheko hicho kinaweza kuwa kibaya au kizuri ila hapa nazungumzia kicheko kizuri cha furaha cha habari njema,Ayubu 8:19-22,Zaburi 126:2,Mwanzo 21:5-7

 

KUHARIBU MIZIMU YA UKOO

Mizimu ni mashetani wanaoendana na mila na desturi za jamii.wachawi wanajuana kutokana na mizimu katika shughuli zako Kutoka 23:32-33,Isaya 8:19,torati 18:10-12

 

RATIBA ZA KISHETANI

Ni utaratibu uliowekwa kwa ajili ya jambo Fulani.Utaratibu huo unawekwa kwa lengo na makusudi Fulani kwa kufuata hatua baada ya hatua.Waamuzi 13:2-5,Waamuzi 13:24,Waamuzi 16:1-3,Waamuzi 16:4---

Yuda,Othnieli,Ehudi,Deborah,Gideoni,Tola,Yairi,Yefta

 

MOYO ULIOJERUHIWA

Moyo kujeruhiwa unatokana na sababu mbalimbali mfano kuachwa,kupigwa,kusalitiwa n.k Mithali 15:13-15 moyo uliyojeruhiwa mtu anakuwa na hasira sana na ugomvi Mithali 15:18,Mithali 15;28,Mithali 15:1,Mithali 16:1

 

MASHAMBA YA KIROHO

Shamba ni sehemu inayotumika kupanda mbegu

Luka 8:5-8

        i.            Njia

      ii.            Mwamba

    iii.            Miiba

   iv.            Udongo mzuri

-Mpanzi ni mtumishi wa Mungu

-Shamba ni moyo

-Mbegu ni Neno la Mungu

Luka 8:11-15,1Wakorinko 3:8-9