KURUDISHA KILICHOIBIWA KIROHO
Kurudisha:Ni hali ya kurejesha kile ulichopoteza,inawezekana ulipoteza mwenyewe au mtu Fulani alikuchukulia au kukuibia na wewe haunacho tena.
Kimsingi Baraka zote zinaanzia katika ulimwengu war oho.Shetani anachokifanya ni kukuibia. Mungu anakuwa ameachilia Baraka zake kwako lakini yupo anayejitokeza anakuibia.
Isaya 42:6-7
Isaya 26:19
Isaya 42:22
ULICHOBEBA NDIYO VITA YAKO
Kuna watu wanafikiri kwasababu ya wazazi wao hawapo,hawana fedha,hawajasoma,hana mtaji,wagonjwa n.k ,hayo yote siyo ni kwasababu ya ulichokibeba ndani yako kutoka Mbinguni
Yeremia 1:4-
-Aliye gizani anaona sana kuliko wa nuruni mfano mama jusi Mathayo sura ya 2
Matendo 9:1-, Matendo 13:9,Zaburi 51:5
-Shetani anaangalia baadhi ya watu muhimu ili awatende mabaya
-Kuna matukio yanakupata wewe,simama nauseme sio hili mfano:Abrahamu,Yakobo aliwaita watoto wake
Gadi:Akamwambia jeshi litamsonga ila yeye atawasonga mpaka visigino Mwanzo 49:19 ,kuna watu wanasongwa kila mahali mfano:kwenye biashara,ndoa,kazini n.k.Yakobo aliona kwenye familia miaka ijayo atatokea mmoja atasongwa na jeshi lakini atalikanyaga mpaka visiginoni
Sifa za Wagadi
-Mashujaa
-Nyuso zao kama samba
-Walikuwa na uwezo wa kupigana vita
-Wepesi milimani
-Walikuwa viongozi wa jeshi
-Aliyekuwa mdogo analingana na watu 100
-Aliyekuwa mkuu (mkubwa) analingana na watu 1000
1Nyakati 12:8-
Shetani anakuona wewe ni mwepesi wa kufanikiwa,ukiachiwa upenyo tu umefanikiwa,ndiyo maana wanasema wakudhibiti na kukusonga lakini saa imefika uwasonge wao mpaka kisigino kwa jina la Yesu.Wana wa Gadi walimiliki ufalme wa Sihoni na familia ya Bashani,Wanefili na mali zao
KUWAFYEKA WATAABISHAJI WETU
Mtaabishaji:Ni mtu au mashetani yanayomzuia mtu asifanikiwe kimaisha.
1Wafalme 18:17
Zimri (Jemedari wa magari) alifanya fitina kwa mfalme (alimpiga),alitawala siku 7(Tirza).Wakaamua Omri Jemedari wajeshi awe mfalme.Alinusuru mji wa Tirza,kukatokea mabishano kati ya Tibni na Omri (alishinda)
Roho ya Yeroboamu alikuwa nayo.Omri alitawala miaka 12 Israel na miaka 6 Tirza alifanya mabaya akafa,akatawala Ahabu miaka 22 akafanya mabaya naye.
KUWAANGAMIZA MAKUHANI WA KISHETANI
Makuhani:Ni viongozi wanaotumika kwenye madhabahu.
Aina za Makuhani
a.Makuhani wa Mungu waefeso 4:11
b.Makuhani wa kishetani Torati 18:10-13 ,Isaya 47:12-15
Tunashindana na binadamu anayetumiwa na mashetani kuharibu maisha yetu
1Wafalme 18:15-40,19:15-27
Wachawi wameloga sana nchi mpaka imegawanyika.Eliya alimfunga lufifa,mashetani ,miungu ,majoka n.k
2Wafalme 10:18-27
MPAKA ILIYOHAMISHWA
Mpaka:Ni alama zinazoonesha eneo la umiliki wa mtu katika ardhi,anga,kwenye maji n.k au ni sehemu,mahali panapoonesha mwisho wa umiliki halali wa mtu.Kuna michoro yake na ramani zake,kuna mipaka ya wilaya,mkoa,nchi n.k.
Mungu baada ya kumuumba mwanadamualimuwekea mipaka yake ya utawala,kutiisha,kumiliki nchi,bahari na anga.Inawezekana kabla ya kuokoka ulikuwa baa mipaka yako ikaamishwa,wachawi wanaweza kuhamisha mipaka ya mtu mfano:kwenye biashara,afya,ndoa,kazi,elimu,fedha,mafanikio n.k Luka 4:1
Unaona hapa shetani hasemi kuwa vyote ni vyangu bali anasema vipo mikononi mwangu.akimaanisha vile alivyonavyo shetani alivipokonya kwa mmiliki wake (mwanadamu).Shetani ndivyo alivyohamisha mipaka.Endapi Mungu alikusudia wewe uishi miaka 120 wachawi hupenda kuipunguza ili usifike umri huo au kuwa waziri,mbuge ukiwa na miaka 40 ukikalibia wanafanya uganga uugue ukose sauti ya kufanya kampeni au uwe Rais,mkurugenzi,daktari,mchungaji n.k lakini ukianza masomo ya kukufikisha huko unashindwa.
Mithali 23:10,Torati 27:17,Hesabu 5:10
Bwana Yesu anaweza kubadilisha tena Kutoka 34:24,Torati 11:24-25
Bwana Yesu anakwenda kuipanua mipaka yako iliyopindishwa kwa jina la Yesu
KUVUNJA ROHO YA UMASIKINI
Umasikini:Ni hali ya kukosa mahitaji muhimu mfano chakula,maradhi,nguo.
Masikini:Ni mtu anayekosa mahitaji muhimu
Kuna umasikini ngazi ya Taifa na umasikini ngazi ya mtu binafsi
Mhubiri 9:14-16,10:19
Shetani anatumia kifungo hiki kuwafunga watu wa Mungu Ufunuo 2:8-9,Mathayo 6:24,Wafilipi 4:19
KUIKOMBOA MIGUU YANGU
Uumbaji wa Mungu,Mtu ni roho.Mtu anasehemu 3 .Shetani naye anawinda sana maeneo hayo
+ Ardhi kwa ajili ya kuujenga ufalme wa Mungu
+ Masikio kwa ajili ya kusikia. Zaburi 103:20
+ Miguu ni milango ya nafsi,ni ishara ya kumiliki eneo,ni kama silaha ya vita
Mithali 6:18,Luka 10:19,Torati 11:24-25,Zaburi 56:6,Ayubu 33:11,Zaburi 57:6
NIMEYASIKIA MAOMBI YAKO
Maombi:Ni mawasiliano kati ya mtu na Mungu kuhusiana na jambo Fulani ili ulipate.
Kiroho:Ni mawasiliano kati ya mtu na Mungu kuhusiana na jambo Fulani ili ulipate
2Wafalme 20:5-11, Matendo 10:30-31
ROHO YA UPATANISHI
Kupatanisha:Ni kitendo cha kuondoa migongano kati ya pande majo na pande nyingine Mathayo 5:9
Baada ya kufa Yoshua waamuzi waliojitokeza:Yuda,Othniel,Elihudi,Debora,Gideoni,Tola Yairi,Yeftha,Samson,Yesu
NGUVU YA NDOTO
Ndoto:Ni picha au matukio yanayotokea kwenye akili yako baada ya kulala Mfano:nimeota ndoto nimenunua gari,ni tumaini/wazo unalokuwa nalo la maisha yako mazuri ya baadae
Aina za ndoto
-Za KiMungu
-Za kishetani
-Za kawaida
Ndoto ina nguvu-nguvu yake ni pale inapotokea kwake.taarifa,maelekezo n.k
Ayubu 33:14,Habakuki 2:2-3
Mfano Yusufu ndoto zake zilitimia.soma Mwanzo sura ya 37
KIFUNGO CHA TANGU UTUTUNI
Kifungo:Ni gereza analofungiwa mtu au kitu kwa sababu za kweli au za uongo
Mhubiri 4:14
Marko 9:17-29
-mtoto wake anapepo bubu
-anampagawisha
-humbwaga chini
-hutuka povu
-kukonda
Walipompeleka kwa Yesu mambo yakatokea
-alipomuona Yesu Yule pepo alimtia kifafa
-akaanguka chini
-akatokwa na povu
Yesu akamuuliza baba yake,amepatwa na haya tangu lini?
-tangu utoto
-mara nyingi amemtupa katika moto,katika maji
-amwangamize
AMEFUNGWA KWENYE MTI
Mti ulitumika kwenye Biblia kama sehemu ya mwisho ya hukumu kwa mtu.Mtu akifungwa kwenye mti baada ya hapo ni kifo,wachawi wanaweza kuutumia mti kama gereza kuyafunga maisha ya mtu au mafanikia ya mtu Yoshua 8:28-29,Esta 7:8-10,2:23,Daniel 4:13-14,Mathayo 27:38-40
KUONDOA VIZUIZI VYA KISHETANI
Vizuizi:Ni vikwazo
Adui wa maisha ya kila mtu ni shetani.shetani ni roho hutenda kazi kupitia mawakala wake ambao ni wachawi,wasoma nyota,waganga wa kienyeji n.k wanauwezo wa kukuua kwenye masomo,elimu,ndoa,kazi,biashara,fedha,maendeleo n.k
1Thesalonike 2:18,Mathayo 8:23-28,Daniel 10:11-14
KUTENGENEZA NJIA KATIKATI YA GIZA
Giza:Ni jambo Fulani lisilokuwa na nuru au lisilo la nuru
Mwanzo 1:1-5,Yohana 1:1-5,Isaya 9:2,Yohana 8:12,Luka 1:79
MWEZI HUU NAPATA NEEMA YA MUNGU
Neema:Ni upendeleo ambao mtu hakustahili kuupata
Luka 1:26
HATA SASA BWANA AMETUSAIDIA
Kusidia:Ni kitendo cha kutoa msaada vile usivyokuwa navyo kuhusiana na jambo Fulani
1Samwel 7:12-14, Mathayo 7:1-,Mathayo 28:1
No comments:
Post a Comment