“Blog ya kukufundisha jinsi ya kupata pesa online kupitia AI, apps, na freelancing.”
Friday, October 10, 2025
UTOFAUTI WA KANISA LA TANZANIA NA MAKANISA YA NCHI ZINGINE
KANISA LA TANZANIA NA KANISA LA NIGERIA TOFAUTI KATIKA WOKOVU, UAMSHO NA UTHUBUTU
Katika kulinganisha maendeleo ya kiroho kati ya kanisa la Tanzania na Nigeria, hoja kubwa imeibuka kwamba Tanzania bado ipo nyuma kwa kiwango kikubwa linapokuja suala la uamsho, uthubutu na mshikamano wa kanisa.
Nigeria: Historia ya Mababa Wenye Uthubutu
Nigeria imejipatia umaarufu mkubwa katika historia ya injili kutokana na watumishi waliolipa gharama kubwa kwa ajili ya wokovu.
Joseph Ayo Babalola (1930): Alitembea mji kwa mji akihubiri injili na kufufua zaidi ya watu 30.
Benson Idahosa: Anatajwa kufufua zaidi ya watu 24 na kufanikisha uamsho mkubwa unaoheshimiwa hadi leo.
Hadi sasa, majina makubwa kama Papa E.A. Adeboye (RCCG) – kanisa linalokusanya zaidi ya waumini milioni moja duniani, David Oyedepo (Winners Chapel) – ibada ikihusisha waumini 250,000 mara tatu kila Jumapili, na Paul Enenche (Dunamis International Gospel Centre) – anayekusanya zaidi ya waumini 100,000 kwa ibada moja, yanaendelea kushuhudiwa. Aidha, majenerali kama Chris Oyakilome, Ayo Oritsejafor, na Apostle Johnson Suleman wameendeleza mwendelezo wa nguvu za injili Nigeria.
Utafiti unaonyesha siri ya mafanikio yao ni umoja, mshikamano, na uthubutu wa watumishi waliotangulia, hali iliyosababisha kizazi cha vijana kurithi neema na kuendeleza huduma kwa urahisi zaidi.
Tanzania: Changamoto za Mgawanyiko na Ubinafsi
Tanzania pia imeshuhudia uamsho kupitia watumishi kama Mzee Moses Kulola, Mwalimu Christopher Mwakasege, Mchungaji Dustan Maboya, na Askofu Kakobe. Hata hivyo, tofauti kubwa iliyojitokeza ni mgawanyiko miongoni mwa watumishi wa injili.
Mara nyingi watumishi wapya walipoinuliwa, walipingwa na waliotangulia kwa kushutumiwa kuwa “pepo” au “shetani”.
Utamaduni huu wa kusemana na kugawanyika umeendelezwa hadi kizazi cha sasa, jambo linalodhoofisha umoja wa kanisa la Tanzania.
Aidha, historia ya uamsho nchini haijarekodiwa kwa kina, tofauti na Nigeria ambapo kumbukumbu za watumishi na matendo yao zimehifadhiwa na kuenziwa.
Swali linaloibuka ni kama Mungu ataikubalia Tanzania kufikia hata robo ya kile kinachoendelea Nigeria. Wengi wanaona bado anga la Tanzania halijashikiliwa kiroho kwa sababu ya roho ya ubinafsi, choyo na ukosefu wa mshikamano wa kanisa.
Wachambuzi wa kiroho wanasema, bila umoja na uthubutu wa kizazi kipya, ni vigumu kuona Tanzania ikipata ukombozi wa kweli wa kiroho, hata ukombozi wa kisiasa.
Nigeria imekuwa mfano wa taifa ambalo kanisa limeinuka na kushikilia anga za kiroho kwa uthubutu. Tanzania, licha ya kuwa na historia ya watumishi waliotumika kwa nguvu, bado inapambana na changamoto za mgawanyiko na ubinafsi.
Ipo haja ya mjadala wa dhati miongoni mwa Wakristo wa Tanzania, hususani vijana, ili kuamua kama wako tayari kulipa gharama na kupindua meza za mgawanyiko kwa ajili ya injili ya Kristo.
MAMBO YANAYOKUFANYA WADHALAULIKE WATUMISHI WA MUNGU
MAMBO YATAKAYO FANYA HUDUMA YAKO KAMA KIJANA KUDHARAULIKA NA WATU AU WATUMISHI WENZAKO
01. KUMKOSA MUNGU KWENYE MAISHA YAKO.
Ukimkosa Mungu , Umekosa Heshima , Ukimshika Mungu umebeba Heshima.
Katika Umri ambao Mungu hutengeneza watu wenye Heshima ni Ujana , Na Katika Umri ambao shetani huwaandaa Vijana wanao onekana watumishi lakini ni wa Hovyo na watazaa aibu Ni Ujanani.
Ikiwa kijana Mungu amekupa nafasi Ya Utumishi mwandame Katika kila siku mpya ili akuheshimishe , Imani yako na Upendo wako kwa Mungu uwe kielelezo kwa watu wote.
02. KUKOSA MAONO YALIYO WAZI KUHUSU NINI MUNGU ANATAKA KWENYE HUDUMA YAKO NA WAPI UNAELEKEA.
Maono ya Kijana Katika Huduma na namna anavyo yaishi maono yake Huleta Heshima , Bali kijana mtumishi asiye na maono kila kitu atataka kufanya , Kila mahali atataka kwenda , Na Kila mtu atataka kumuiga , Na Kila style ya maisha atataka kuishi kwa sababu Hana maono :
NB: Maono Kwa Kijana yanampa Nguvu ya Kufocus na Nguvu ya Kuzaa matokeo yenye Tija Yanayoshikika.
03. KUMFANYA KILA MTU MZAZI WAKO WA KIROHO NA MENTORS KILA MAHALI.
Moja ya Baa kubwa linaloleta dharau kwa vijana wengi ni Kutaka kila mtu maarufu awe baba yake wa kiroho , Kila mchungaji maarufu mtandaoni ni mentor wake na mlezi wake ,
Katika maisha ya kawaida tu mtoto anayekula kula kwa watu anaitwa mlafi na mwenye tamaa , Watumishi wengi vijana wanaonesha tabia ya tamaa kwa kufikiri kuwaita wachungaji maarufu ni mababa zake , Unatoka baba X kwenda Y , Kesho uko kwa Baba A , Tena unahama unaenda kwa baba H
NB: UTULIVU HULETA HESHIMA KUTANGA TANGA HULETA DHARAU
04. KUDEKA DEKA KWA WATU ILI WAKUONEE HURUMA KAMA WEWE NI MTUMISHI WA MUNGU.
Watu watakuheshimu kwa kadiri unavyo onesha kumtegemea Mungu kupo kwa Namna Gani.
Tupo katika kizazi ambacho vijana wengi wapo kwenye Huduma na hawajui mipaka yao kwa washirika au watu , Unakuta mtumishi wa Mungu kijana amejaza inbox za watu akiomba omba fedha au anatembelea watu kueleza shida zake ili aonewe huruma , Huo ni Utoto wa kiroho acha haitakujenga.
05. KUOMBA OMBA WATU PESA INBOX, HASA PESA ZA MATUMIZI YAKO BINAFSI KAMA CHAKULA , KODI YA NYUMBA AU MAVAZI.
Ni fedheha mtumishi wa Mungu Kuomba Omba kwa watu chakula , Mavazi au kodi Ya Nyumba , NI BORA SANA KUMUOMBA MUNGU. Ni Mbaya sana kwa mtumishi wa Mungu kuwalemea watu katika kupata mahitaji yako Bonafsi.
2 Corinthians 11:9
“9.Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu; nami katika mambo yote najilinda nafsi yangu nisiwalemee hata kidogo; tena najilinda.
06. KUKOSA UTARATIBU NDANI YA KANISA, IBADA ISIYO NA UTARATIBU INALETA DHARAU KWA KIONGOZI WA KANISA.
1 Corinthians 14:40
Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.
07. KUWA NA WASAIDIZI WALIOKOSA AKILI AU MAARIFA YA HUDUMA [ WATU HAWA WANAWEZA KUKURUDISHA NYUMA KILA SIKU].
Kila msaidizi unayemuweka kwenye Huduma yako ni sura yako na maonyesho ya tabia zako,
Msaidizi mwema kwenye Huduma atakuletea heshima bali msaidizi mbaya atakuletea Mavuno ya dharau kwenye Huduma yako, Chagua kwa hekima na Uongozi wa Roho Mtakatifu mtu anayeweza kukukaimu majukumu Yako au anayeweza kusimama na wewe Vema .
08. KUMDHARAU MUME AU MKE WAKO KUTAFANYA HUDUMA YAKO IDONDOKE KABISA.
Waebrania 13:4
4.Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.
09. KUVAA VIBAYA NI NYAVU YA KUVUA DHARAU .
Moja ya mtego mdogo ila wenye kuvuna dharau nyingi ni Mavazi, Kuna watu walikuwa wanaheshimika vema kabisa ila mpaka walipovaa mavazi fulani,
Mavazi yanaweza kuleta aibu au heshima, Mpangilio wa Uvaaji wako unaweza kuleta heshima au dharau ,
NB: Mavazi ni Jambo la Kiroho sana Usipuuze.
10. KUPOST MAMBO YASIYO FAA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII NA KUENDANA NA UADILIFU WA HUDUMA HUONGEZA DHARAU.
Kila jambo ambalo unalifanya kupitia mitandao ya kijamii linaweza kukuweka kwenye kundi la watu watakao pokea heshima au wale watakao pokea dharau,
Mitandao ya kijamii inaweza kuvuta watu heshima wakuheshimu au watu wenye dharau wakudharau.
11. KUAMBATANA NA WATUMISHI WASIO NA MAADILI NA WASIOTAKA KUBADILIKA HATA WAKIONYWA.
Mithali 13:20
“20.Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.”
12. KUKOPA WASHIRIKA WAKO FEDHA AU KUWALAZIMISHA WAKUPE FEDHA ,
Mtumishi kijana anayekopa kopa washirika fedha Huishia kwenye fedheha na dharau kabosa ,
Fikiri kidogo , Mchungaji madhabahuni unahuburi halafu mshirika anakudai yuko kanisani anakusikiliza ukisema pokea fedha , Mshirika anawaza nikitoka hapa namdai , Na Mchungaji unachukua sadaka kila siku kulipa madeni ambayo ulipata kwa sababu ya matumizi binafsi. NI AIBU.
NB: EPUKA KUKOPA WASHIRIKA AU KUWALAZIMISHA WAKOPE ILI WAKUPE WEWE FEDHA
WEWE NI KIJANA, UNA NDOTO ZA KUWA MTUMISHI WA MUNGU, HII NI FURSA YAKO.
AINA YA WASHIRIKA WASUMBUFU KANISANI
AINA ZA WASHIRIKA WAKOROFI KWENYE MAKANISA YENYE WACHUNGAJI VIONGOZI VIJANA
01. WASHIRIKA WASIOTAKA MAOMBI WALA KUJIFUNZA NENO LAKINI WANATAKA UWAPE NAFASI YA KUFUNDISHA NA KUHUBIRI KILA MARA.
Washirika Hawa Hupenda sana kuonekana na Kujionyesha kuwa wanajua hata kama hawajui.
Washirika wa jinsi hutawakuta kwenye maombi , Madarasa ya neno au mikusanyiko ya vikundi kanisani ila wakija wanataka Uwapishe uwaachie madhabahu.
NB: Ukiwapa Nafasi washirika kama hawa kanisani Unatengeneza washirika wasiojali sauti ya Mchungaji wao, Na Wengi huangukia Mafunuo Batili Na Ujanja ujanja wa kidali katika Huduma.
02. WASHIRIKA WAPINGA UONGOZI , LOLOTE KIONGOZI ANALOSEMA WAO WAPO KINYUME NAO.
Aina hii ya washirika ni Hatari sana mfano wake ni Kora , Dathani na Abiramu , unaweza kusoma habari zao kutoka katika biblia kitabu cha Hesabu, Washirika wa jinsi HUTENGENEZA MIKUSANYIKO KINYUME NA MCHUNGAJI
Hesabu 16:1-3.
1. Basi Kora, mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, akatwaa watu, pamoja na Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu, na Oni, mwana wa Pelethi, waliokuwa wana wa Reubeni;
2. nao, pamoja na watu kadha wa kadha wa wana wa Israeli, watu mia mbili na hamsini, Wakuu wa mkutano, waliokuwa wateule wa mkutano, watu wenye sifa, wakainuka mbele ya Musa;
3.nao wakakusanyika kinyume cha Musa na Haruni, na kuwaambia, Ninyi inawatosha, kwa kuwa mkutano wote ni mtakatifu, kila mmoja miongoni mwao, BWANA naye yu kati yao; n’nini basi kujitukuza juu ya mkutano wa BWANA?
NB: Mchungaji wa kanisa la mahali pamoja Ukiona watu kama Kora usiwape hata nafasi ya kusimama mbele au Kuongea na washirika , Watu hawa lolote wanalofanya lengo lao mwishoni ni Kuiba na kuigeuza mioyo ya washirika kinyume cha mchungaji wao.
03. WASHIRIKA WANAOMCHUKULIA MCHUNGAJI KIONGOZI KAMA KIJANA WAO , HIVYO AKILETA MAONO WANAMWITA PEMBENI KUMKEMEA NA KUMWAMBIA UWE TARATIBU HAYO MAONO NI MAKUBWA.
Mara nyingi washirika wa jinsi Hii huwa wanahisi kwa sababu ni wakubwa kiumri basi wanatakiwa kumuongoza mchungaji na kumuamuru nini cha Kufanya , washirika kama hawa hupenda kuita makanisa yenye viongozi vijana kama makanisa ya watoto.
Kuna wakati Petro aliona kama Yesu anakosea mafundisho yake kwa kueleza kuwa kuna siku atakufa na kufufuka akamwita pembeni akamkemea kiongozi wake ,
Matthew 16:21-23
21.Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka.
22.Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.
23.Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu. Msalaba na Kujikana
NB: Washirika Wa Jinsi Hii Wape nafasi ya kuwasikiliza na Kuyapima mashauri yao kama yatakupigisha hatua katika Huduma au La.
04. WASHIRIKA WANAOJUA KUTOA AHADI ZA MICHANGO TENA MIKUBWA WANAONGEZA MATUMAINI KWENYE MALENGO YA KIFEDHA KATIKA MIRADI YA KANISA LAKINI HAWATOI , LENGO LA HUWA NI KUPATA SIFA TU.
Ogopa sana ikiwa watu hawa wakatoa ahadi na wasizitimize wanakatisha tamaa wengine kutoa hata kama walikuwa wanatoa kidogo.
MITHALI 20:25
“Ni mtego kwa mtu kutamka kwa haraka neno la nadhiri, kisha baadaye kufikiri juu yake.”
NB: Ukiwajua washirika wa Jinsi Hii Usiwape nafasi ya Kuahidi Tena kama hawaondoi nadhiri zao hii ni njia Ya Kuwalinda na Kuwapa nafasi ya Kujitathimini.
05. WASHIRIKA WANAOTONGOZA WAPENZI WAPYA KILA SIKU NA WANALETA KUTAMBULISHA KWA MCHUNGAJI LAKINI HAWAOI.
Washirika wa jinsi Hii huwa na mioyo myepesi katika kuanzisha mahusiano na kutoka mwishowe hutengeneza makovu kwa washirika yasiyopona.
Katika kizazi cha sasa jambo hili si kwa vijana tu bali hata mabinti anaanza mahusiano na kijana akiona hana pesa anampiga chini anaanza mahusiano mengine mapya, Hakuna Uaminifu , KANISA LINAJAA WASHIRIKA WENYE MAGONJWA NA VIDONDA VYA MAHUSIANO.
06. WASHIRIKA WANAOJUA TAARIFA ZA WASHIRIKA WOTE KANISANI NA KAZI YAO KUBWA NI KUTOA MAELEKEZO KWA WASHIRIKA WAPYA KWA KUSEMA HABARI ZA NDUGU ZAKE.
Mithali 20:19
19. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.
“Mchongezi Hueneza Siri, basi usishirikiane naye azidishaye midomo yake.”
07. WASHIRIKA WAKOPAJI , KILA MTU KANISANI ANAKUWA ASHAKOPWA NA HALIPI.
Psalms 37:21
“21.Asiye haki hukopa wala halipi, Bali mwenye haki hufadhili, hukirimu.”
Hawa utawasikia wanasema Una Laki Hapo nitumie mara moja jioni kuna mchongo nausikilizia nakurudishia , Kwa sababu ni mpendwa Unampa Baada ya Hapo Harudishi, Hapokei simu , Hajibu sms , Akija kanisani anakuwa wa kwanza kuondoka asikutane na mtu.
Watu wa jinsi wakikutana na mshirika tajiri kanisani wanampiga kitu kizito mpaka mshirika anahama mpaka umegundua hilo tatizo ushapoteza washirika wapya wa maana.
NB: Usizoee kukopesha wapendwa ni Bora utoe kama sadaka ili kudumisha umoja
08. WASHIRIKA WASIOJALI WANAVYO VAA WAKIDAI MUNGU ANAANGALIA ROHO TU :
Washirika hawa hupenda mavazi yanayowaonesha maungo yao , Na ukiwasema tu unaonekana mchungaji una changamoto , Washirika Hawa Huwa na nguvu sana ya kuwavuta vijana wajinga kwa tamaa,
1 Timothy 2:9
“9.Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi.”
NB: Unaweza Usijali Kuhusu mavazi kama mchungaji lakini Watu ambao tumeitwa kuwa nuru kwao Wanajali na wanalitambua kanisa kwa namna mnavyo vaa Pia.
09. WASHIRIKA WANAOLIGAWA KANISA , ENDAPO KUNA WAHUDUMU ZAIDI YA MMOJA.
Washirika kama Hawa hutengeneza makundi ndani ya kanisa , Utakuta wako wanaosema mimi simuelewi mchungaji namuelewa mzee fulani , Wengine wanasema mimi simuelewi Mtu fulani akiongoza sifa , [ WASHIRIKA HAWA HULIGAWA KANISA NA KUFANYA KANISA LISITAWALIKE]
1 Corinthians 1:12-13
“12.Basi, maana yangu ni hii, ya kwamba kila mtu wa kwenu kusema, Mimi ni wa Paulo, na, Mimi ni wa Apolo, na, Mimi ni wa Kefa, na, Mimi ni wa Kristo.
13.Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulibiwa kwa ajili yenu? Au je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?”
Washirka hawa hutumia Fedha na mali katika kuimarisha makundi yao ndani ya kanisa, Mchungaji asipokuwa makini washirika hawa huweza kulipasua kanisa au kufanya kanisa lisitawalike kabisa na Huduma kuwa ngumu.
10. WASHIRIKA WANAOPENDA KUFUATILIWA SANA NA KUPEWA AHADI NYINGI ILI WAJE KANISANI.
Washirika wa jinsi wanapenda mchungaji uwapigie simu kila wakati , uwatumie message na uwape Ahadi nono kabla hawajaja kanisani na usipofanya hivyo Unakuta hawaji kabisa kanisani , Kabla ya siku ya ibada wanataka usiku uwapigie simu , wanachosha sana hawa.
Aina hii ya washirika wanapenda wakija kanisa uwape ahadi za chakula , Juice au nyama choma ili waje kwenye ibada au mikesha ,
NB: Mchungaji mzembe Huwazoesha washirika wa jinsi Hii Na Kutengeneza kanisa na washirika dhaifu wasioweza Kujisimamia .
Thursday, October 9, 2025
Thursday, May 15, 2025
BEELZEBURI (Mkuu wa mapepo)
BEELZEBURI (Mkuu wa mapepo)
Beel maana yake ni mkuu/bwana
Zeburi maana yake ni mapepo wachafu
Beelizeburi ni shetani anayesimamia mapepo yote
kwa kuyapa amri Marko 3:20-30,Mathayo 12:22-24,Luka11:24.Mapepo tabia zao ni
anataka kuishi sehemu ambapo hapana maji (makavu/pakavu) pasipo na maji maana
yake ni moyo mkavu-Roho Mtakatifu hayupo,na mapepo hayana makao maalumu
yanasubilia kualikwa/kuitwa Marko 16:9,nchi ya Wagerasi Marko 5
AMEFUNGWA KWENYE MTI
Mti
ulitumika kwenye Biblia kama sehemu ya mwisho ya hukumu kwa mtu.Mtu akifungwa
kwenye mti baada ya hapo ni kifo.wachawi wanaweza kuutumia mti kama gereza
kuyafunga maisha ya mtu au mafanikio ya mtu Yoshua 8:28-29,Esta 7:8-10,2:23,Danieli
4:13-14,Mathayo 27:38-40
Maombi
-kuwapiga
waliokufunga kwenye mti
-kushuka
kwenye mtu
KUONDOA VIZUIZI VYA KISHETANI
Vizuizi ni vikwazo
Adui wa
maisha ya kila mtu ni shetani,shetani ni roho hutenda kazi kupitia mawakala
wake ambao ni wachawi,wasoma nyota,waganga wa kienyeji n.k wanauwezo wa kukaa
kwenye masomo,elimu,ndoa,kazi,biashara,fedha,maendeleo 1Wathesalonike
2:18,Mathayo 8:23-28,Danieli 10:11-14
Maombi
-kuwapiga
wanaokuzuia
-kuondoa
vizuizi
SAA INAYORUDI NYUMA
Saa ni kifaa
kinachoonesha mudauliopo.Kuna saa za analogia na kuna saa za kidigitali.Kuna
saa za asubuhi,kuna saa za mchana,kuwa saa za jioni,kuna saa za usiku.Zamani
hata sasa walikuwa wanatumia jua,mwezi,sauti Marko 14:32-42,Mathayo
27:45-50,Mathayo 10:19-20,Mathayo 24:36,25:13.Shetani anaweza kuiona saa yako
badala ya kwenda mbele yeye anairudisha nyuma au anaisimamisha mfano
biashara,kazi,familia,elimu.Anakuwekea saa feki,
BADILI LUGHA YAKO
Maana ya
lugha.Kuna lugha ya mazungumzo,maandishi,vitendo,picha.Kila nchi ina lugha yake
ya taifa,lugha ndiyo chombo cha mawasiliano mfano mke na mume.Lugha ndiyo nguvu
ya mahusiano 1Wakorintho 13:1
Lugha za
wanadamu,za malaika,mashetani
Kunena kwa
lugha ndiyo lugha ya ufalme wa Mungu lakini unaponena kwa lugha inapaswa moyo
wako uwe safi unaweza ukawa unaongea vitu vingine kwa Mungu au shetani akatumia
kinywa chako,hapa unapaswa kuwa makina sana.Matendo 2:1-4,Warumi
8:26,1Wakorintho 14:2.Sema nabadilisha lugha ya
magonjwa,umasikini,shida,balaa,laana,mikosi,kushindwa n.k juu ya maisha yangu
kwa jina la Yesu Kristo
KUONDOA ROHO ZA HASIRA
KUONDOA ROHO ZA HASIRA
Hasira ya
mtu siku zote haitendi haki.Na hasira inaendana na vitu vitatu,moyo,akili na
matendo.Hasira inaweza ikafanya maamuzi mabaya yaani haitendi haki hata mara
moja.Siku zote ukiwa na hasira jaribu kujidhibiti,usifanye jambo baya au
kufanya maamuzi mabaya na kamwe usiongee maneno mabaya siku zote Yakobo
1:20,Waefeso 4:26,Mhubiri 7:9,Mithali 19:11,Mithali 15:1,18,Mithali 14:17
MTAABISHAJI WA MAISHA YAKO
Mtaabishaji
linatokana na neno taabika.Mtaabishaji ni mtu anayeumiza,teas,haribu,anayekukosesha
amani,anayekukosesha raha n.k 1Wafalme 18:17-------
MTI WA KIROHO
Mathayo
13:31-32
Mti ni mtu
Ndege ni neno
Shamba ni moyo
Mungu
anapanda mbegu kwa Yesu (amepanda ndani ya moyo wa Yesu).Yesu alikuwa mdogo
sana kwa Wayahudi,Yesu akakua mpaka mtu mkubwa.Mbegu ni ndogo lakini inathamani
kubwa sana Isaya 55:12
ROHO ZA URITHI
Urithi ni
hali ya kumilikishwa kitu au vitu
Aina za urithi
·
Urithi
wa Kimungu
·
Urithi
wa kishetani
Urithi
waKimungu
Yushua
19:49,Isaya 54:17---,Zaburi 127:3,Zaburi 16:6-8,Zaburi 33:12,Mithali
13:22,Mithali 19:14,Yeremia 3:19
Urithi wa
kishetani
Yeremia
12:8-9,Mathayo 21:38-39
KUANGUSHA BABELI YA KIROHO
Babeli ni
mji wa zamani ulikuwa umejengwa huko Mesopotamia mashariki ya kati 2Wafalme
24:11,Babeli ni gereza linalowashikilia watu.Isaya 21:9,Ufunuo 14:8,Ufunuo
17:1-18,Ufunuo 18:21
KUHARIBU ROHO ZA LAANA
Laana ni
mkusanyiko wa mambo mabaya yanayompata mtu
Kuna laana
ya ardhi na kuna laana ya mtu.Kinachobeba laana mpaka iwe na nguvu ni
·
Maneno
Torati 29:19
·
Kafara
1Wafalme 2:8
·
Kiapo
Zaburi 10:7,Warumi 3:14
LUCIFER DNA
Vinasaba vya
shetani.Ni chembechembe ndogo ambazo hubeba taarifa zote za kibaiolojia kwa
kila kiumbe(urithi) yaani uzao 1Yohana 3:10---,Mwanzo 6:1-4,Torati
2:20.Wanasayansi walishawai kugungua vinasaba vilivyochanganyikana na binadamu
KURA HUKOMESHA MASHINDANO
KURA HUKOMESHA MASHINDANO
Kura ni
kuchagua mtu au kitu,Matendo 1:23-26,Mithali 18:18,Mithali 16:33
UNAONA NINI?
Katika
maisha watu wengi wamefichwa macho ya rohoni.Ninapozungumzia macho,nazungumzia
·
Ufahamu,uzima,afya,uweza
·
Fikra,kumtafuta
Yesu
·
Akili
·
Nguvu,maono
yako
·
Hatua
·
Mafanikio
Yeremia
1:11-12,Yeremia alikuwa kuhani(mmoja wa makuhani)kwenye nchi ya
Benyamini.Nenola BWANA lilimjia wakati wa kutawala kwake mfalme Yosia (Mfalme
wa Yuda) Hesabu 13:33,Hesabu 14:6-10
MUNGU AKUKUMBUKE TENA
Kukumbukwa
ni hali ya kuonekana kwa mtu/kitu(kutolewa/kukubaliwa) ulikuwa umesahaulika
sasa umeonekana Mwanzo 8:1---.Mungu alimuambia Nuhu ajenge safina,urefu mikono
300
,upana
mikono 50
,urefu
kwenda juu mikono 30
.Tarehe
17/02/600 mvua ikaanza kunyesha mpaka
tarehe 26/03/600 mvua iliacha.Maji yalitulia
siku 150 (miezi 5),
tarehe
17/07/600 safina ikatua mlima Ararati (Uturuki ya leo)
,tarehe
01/10/600 maji yalipungua pungua
,tarehe
07/10/600 alimtoa kunguru na njiwa,
tarehe
14/10/600 alimtoa njiwa,
tarehe
01/01/601 nchi ilikuwa kavu
,Mungu
akamwambia Nuhu toka kwenye safina
WAZAZI WETU WALITENDA MAOVU
Maombolezo
5:7,Yeremia 16,Mhubiri 3:1,Mhubiri 9:11
WAKATI NA BAHATI UWAPATA WOTE
Bahati ni
kukipata kitu bila kutegemea au kuepuka kitu ambacho hukutegemea.Mhubiri
9:11,Mhubiri 11:5-6
BONDE LA MATESO
Mateso ni
matatizo yaliyopo ndani au nje ya mtu Luka 3:1-6
JITAMKIE UNABII
Unabii ni kitendo cha
kutabiri,yaliyopo,yaliyopita,yaliyopo na yanayokuja
Nabii ni mteule/mteuliwa wa Mungu aliyeitwa
kupeleka ujumbe kwa watu.1Wakoritho 12:10,2Petro 1:20-21,Ufunuo 1:1-3,Ufunuo
1:19
KUFUTA PICHA ZILIZOKUWA KWENYE AKILI
YAKO
Katika
maisha kuna mambo yamesimama kama picha mbaya,inaweza ikawa
ugonjwa,umasikini,taabu,mateso,balaa n.k 1Samweli 17:1-5
·
Goliath
alikuwa na urefu futi 6
·
Chepeo
ya shaba shekel elfu 5
·
Mabampa
miguuni
·
Mkuki
kwenye begani
1Samweli
17:42---,1Samweli 18:6,Hesabu 13:17,hesabu 14:1
UVUNJA ROHO ZA SODOMO NA GOMORA
KUVUNJA ROHO ZA SODOMO NA GOMORA
Sodoma na
Gomora hii ilikuwa ni miji iliyokuwa ikitenda mambo mabaya mbele za Mungu,kwa
wanaume kuwakiana tama na wanawake vile vile kuwakiana tama yaani kwenda
kinyume na maumbile.Kutumia miili yao kinyume na asili ya viungo vya uzazi kwa
matumizi yake.Mwanzo 13:13,Warumi 1:26-27,Warumi 1:24-25,Warumi1:28-32,Mwanzo
18:1-15,Mwanzo 19:4-11
HATA WAKUZUIE UTAVUKA
Torati
9:1-5,Torati 11:30-30,Marko 4:35-41,Marko 5:1---,Matendo 16:9-21
Kushukuru
Zaburi 50:23,Wafilipi 4:4-7
-kusali
–prayer
-kuomba-
supplication
-kushukuru-
thanksgiving
(humbly,begging,asking)
JIUNGANISHE NA MADHABAHU YAKO
Madhabahu
(Altare,Alta) ni sehemu yoyote ile mtu anapokutana na roho inaweza kuwa ni roho
ya Mungu au shetani
Ndani ya madhabahu kuna
·
Kutoa
sifa-nyimbo
·
Kutoa
sadaka
·
Kuomba
(kupeleka mahitaji)
Ezra 3:1-6
Faida ya madhabahu
·
Ni
upatanisho
·
Inafungua
Baraka
·
Inatupa
ulinzi wa Ki-Mungu Mwanzo 8:18-22
·
Madhabahu
inasema mbele za Mungu
·
Inamdhihirisha
Mungu unayemuabudu
KUVUNJA ROHO YA TALAKA
KUVUNJA ROHO YA TALAKA
Talaka ni hati ya kiapo cha kuvunja ndoa
Aina za ndoa
i.
Ndoa
ya kidini yaani ya Kikristo na Kiislamu
ii.
Ndoa
ya kiserikali
iii.
Ndoa
ya kimila
Mwanzo 2:24
Ndoa na iheshimiwe Waebrania 13:4
Madhara ya talaka
·
Kuzuia
hatima za watoto wenu zisitimie kwa wakati
·
Kuleta
magonjwa
·
Familia
kusambalatika
·
Heshima
itapungua
·
Kuyumbisha
watoto
·
Kuleta
mauti
Marko
10:4-12,Malaki 2:16
Maagizo ya ndoa
1Wakorintho 7:1-6,1Wakorintho
7:8-16,1Wakoritho 7:33-34,7:39
WAKUACHE UONEKANE
Ili mtu
ufanikiwe kwenye jambo Fulani ni lazima aonekane,iwe kibiashara,kindoa,kikazi
n.k Wafilipi 3:9-10,Mithali 17:8,Mhubiri 6:4
VINYAGO VYA BABAYE
Vinyago ni
miungu inayoabudiwa au ni sanamu zinazoabudiwa kulingana na jamii husika,kuna
miungu ngazi mbalimbali mfano kwenye familia,ukoo,kwenye wilaya,mkoa,kitaifa na
kimataifa,inaabudiwa sehemu mbalimbali kama vile ofisini,nyumbani.Kutoka
20:1-6,Torati 6:14-15,Mwanzo 31:19,Mwanzo 35:2
HAKUNA ATAKAYESIMAMA MBELE YAKO
MASHIMO YA KICHAWI (Kiroho)
MASHIMO YA KICHAWI (Kiroho)
Agano la
kale mtu alipokuwa anafanya kosa au makosa alikuwa anahukumiwa kwa kutupwa
kwenye mashimo marefu.
Mashimo yaliyokuwepo
i.
Mashimo
yenye wanyama mfano Danieli
ii.
Shimo
lenye moto mfano Shedraka,Meshaki na Abednego
iii.
Shimo
lenye maji mengi au matope mfano Yeremia 38:6
iv.
Shimo
lisilo na kitu
Sasa
Shetani naye
vile vile naye ameyaweka mashimo yake haya kwa namna ya kiroho,hayaonekani kwa
macho ya kawaida kwasababu shimo lenyewe ni roho kamili,lina akili,linaweza
kukimbia na ukiingia ndani huwezi kutoka linageuka na kuwa giza.Zaburi
35:7,Ufunuo 9:1-2,Isaya 24:17,14:15,Isaya 38:18
Miji inaweza
kuwa na mashimo ya rohoni na utakaposhughulika na shimo hilo unakuwa umeuteka
mji.Kuna mashimo makubwa yaani kuzimu ya
angani,kuzimu ya baharini ,kuzimu ya nchi
Pia kuna
vishimo vidogo mfano mtu anachukuliwa msukule na kuwekwa
kabatini,kisimani,dukani,n.k Isaya 42:22
Kila mtu
amewekewa Baraka zake sehemu Fulani mfano kwenye
kinywa,tumbo,kumbukumbu,biashara,ndoa n.k
Familia,ukoo
wanawekwa kwenye mashimo ya
mauti,magonjwa,laana,mikosi,shida,balaa,utasa,umasikini n.k
Mambo unayotakiwa kuyafahamu kuhusu
kuzimu
i.
Malaika
wa kuzimu ufunuo 9:11
ii.
Makomeo
ya kuzimu Ayubu 17:16
iii.
Milango
ya kuzimu Ayubu 38:17,Mathayo 16:18
iv.
Kamba
za kuzimu 2Samweli 22;6
v.
Makao
ya kuzimu Zaburi 89:88
vi.
Shida
za kuzimu Zaburi 116:3
vii.
Kitanda
cha kuzimu Zaburi 139:8
Maombi
-kuyashambulia mashimo yote ya kichawi
-kuwateketeza walinzi wa mashimo
-kutoka shimoni
ROHO YA MPINGA KRISTO
ROHO YA MPINGA KRISTO
Maana yake
ni kwenda kinyume na Kristo au kugeuza ukweli wa Yesu Kristo kuwa uongo.1Yohana
2:18,1Yohana 2:22,1Yohana 4:1-3,2Yohana 1:7,2Wathesalonike 2:4,Mathayo 10:16
Dalili za roho ya mpinga Kristo
zinazonyemelea mtu/watu
i.
Kulizoea
Neno la Mungu
ii.
Kutokumuamini
Yesu
iii.
Kumkana
Yesu Kristo
iv.
Kuchukia
mambo ya Mungu mfano maombi
v.
Kuanza
kuamini vitu ambavyo sio vitu vya Kimungu
vi.
Kufanya
uovu bila kuumia moyoni
vii.
Kutokusamehe
na kuachilia 1Yohana 4:20-21
viii.
Kutokuzifuata
sheria na kanuni za Yesu Kristo
MTUMAINI BWANA
Tumaini
maana yake kumtegemea Mungu Baba Mithali 3:5-10
·
Kwa
moyo wako wote
·
Usizitegemee
akili zako mwenyewe
·
Katika
njia zako mkiri (mtaje Yesu/Mungu)
·
Usiwe
mwenye hekima machoni pako mwenyewe
·
Utajiepusha
na uovu
·
Mheshimu
BWANA kwa mali zako
KUIPINGA ROHO YA UMASIKINI
Umasikini ni
hali ya kupungukiwa .Kuna umasikini wa mtu binafsi na kuna umasikini wan
chi,kata,tarafa,mtaa n.k Torati 15:4----,Torati 15:7,Mwanzo 13:2,Mithali
19:17,Yakobo 1:27
NIMEWEKA MLINZI
Ezekieli
3:17,Danieli 4:13,Zaburi 121:4-5,Zaburi 141:3
KUFUTA MASHIMO YA KIROHO
Zaburi
119:85,Yeremia 2:6,Waebrania 11:36
UNAJULIKANA MBINGUNI
Kujulikana ni hali ya kufahamika
·
Kufahamika
na Mungu
·
Kufahamika
na wanadamu
·
Kufahamika
na mashetani
Yeremia
1:4-10
Faida za kujulikana na Mungu
·
Utapata
msaada/watakusaidia
·
Utazawadiwa
·
Utapata
kibali
·
Utapata
neema
NABII WA MATAIFA
Nabii ni
sauti ya Mungu duniani anayepewa ujumbe na Mungu kupeleka kwa wanadamu Yeremia
1:4-10,Hesabu 12:6,Torati 34:10,Waamuzi 4:4








